Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akisalimiana na Balozi wa Cuba nchini, Mhe. Jorge Luis Lopez Tormo,
kabla ya mazungumzo yao, ofisini kwake jijini Dar es slaam Januari 11,
2016. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akizungumza na Balozi wa Cuba nchini, Mhe. Jorge Luis Lopez Tormo,
ofisini kwake jijini Dar es slaam Januari 11, 2016. (Picha na ofisi ya
Waziri Mkuu)
………………………………………………………………
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa
amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Cuba nchini, Bwana Jorge
Luis Lopez Tormo ambaye ameahidi kuendelea kusaidia Tanzania katika
mapambano dhidi ya malaria.
Akizungumza na Balozi Tormo leo
,ofisini kwake ,Magogoni jijini Dar es salaa, Waziri Mkuu amemshukuru
Balozi huyo, kwa Serikali ya Cuba kuendelea kusaidia Tanzania
katika mapambano dhidi malaria kwa kusaidia ujenzi wa kiwanda cha
kwanza Afrika cha viuadudu vya kuua viluwiluwi wa mbu wanaoeneza
ugonjwa wa malaria kilichopo, Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani
kinachosimamamiwa na Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC).
“Nawashukuru sana kwa namna
mnavyosaidia kupambana na malaria, kupitia mradi huo mkubwa Afrika ambao
unalenga kumaliza ugonjwa wa malaria,unaosababisha idadi kubwa ya vifo
katika nchi yetu.” alisema Waziri Mkuu Majaliwa.
Pia, ametumia fursa hiyo
kuwakaribisha raia wa Cuba kuja kuwekeza nchini hasa
katika teknolojia. Na ameahidi kuendeleza uhusiano mwema ulipo baina
ya nchi hizi mbili.
Waziri Mkuu ameendelea kwa
kusema kuwa Cuba ni nchi iliyoendelea katika biashara, viwanda na
uwekezaji na imefanikiwa kutoa bure huduma za kijamii ikiwemo afya,
hivyo Serikali ya Tanzania haina budi kujifunza kutoka kwao ili kutimiza
azma yake ya kutoa bure huduma mbalimbali za kijamii kama ambavyo sasa
inatolewa elimu bure.
Kwa upande wake, Balozi Tormo
amesema kuwa pamoja na Serikali ya Cuba kusaidia kutoa wataalamu
katika kujenga kiwanda hicho cha viuadudu vya kuua viluwiluwi wa mbu
wanaoeneza ugonjwa wa malaria ambao utanufaisha pia nchi za jirani siku
za usoni, wanapenda kuendeleza ushirikiano na Tanzania katika kuzalisha
wataalamu kupitia programu mbalimbali ikiwemo afya na elimu. Mfano
progamu inayoendelea ya kubadilishana wataalamu katika kitivo cha
madawa cha Chuo Kikuu Cha Zanzibari (SUZA).
“Tunaweza kuendeleza program za
kujifunza lugha ya Kiswahili, kama hapo awali, hii ni njia nzuri na
muhimu ya kuendeleza uhusiano wetu na watu kuelewa lugha zetu”, alisema
Balozi Tormo.


0 comments :
Post a Comment