TAIFA STARS YAANZA MAZOEZI
KIKOSI
cha Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kimeanza mazoezi katika
uwanja wa Karume kujiandaa na mchezo dhidi ya Nigeria kuwania kufuzu kwa
Fainali za Mataifa ya Afrika mwaka 2017 nchini Gabon.
Wachezaji
wa Taifa Stars chini ya kocha wake mkuu Charles Mkwasa watakua
wakijifua mara mbili kwa siku asubuhi na jioni katika uwanja wa Karume
katika kujiweka fit na maandalizi ya mchezo huo.
Kufuatia
baadhi ya wachezaji kuwa na majukumu na timu zao kujiandaa na mchezo wa
Ngao ya Hisani utakaochezwa Agosti 22, Mkwasa amewaongeza wachezji
wengine kumi (10) kutoka katika orodha yake ya akiba.
Lengo
la kambi hii ya awali ya siku tano, ni kocha mkuu pamoja na benchi lake
la ufundi kupata nafasi ya kuwaona wachezaji katika mazoezi hayo kabla
ya safari ya kuelekea nchini Uturuki Agosti 23 mwaka huu kwa kambi ya
siku kumi.
Wachezaji
walioitwa na kuanza mazoezi leo ni Said Mohamed, Vicent Andrew (Mtibwa
Sugar), Mohamed Hussein, Ibrajim Hajibu (Simba SC), Hamis Ali, Juma
Mbwana (KMKM), Tumba Sued (Coastal Unioni), Samuel Kamuntu (JKT Ruvu),
Ibrahim Hilka (Zimamoto– Zanzibar) na Mohamed Yusuf (Prisons).
Wachezaji
wengine waliopo kambini ni Said Ndemla, Hassan Isihaka, Abdi
Banda(Simba SC), Rashid Mandawa (Mwadui FC), Michael Aidan (Ruvu
Shooting), Orgeness Mollel (Aspire Academy) na Abdulhaman Mbambi
(Mafunzo).
TWIGA STARS KUIVAA HARAMBEE STARLETS
Timu
ya Taifa ya Tanzania ya Wanawake (Twiga Stars) iliyopo kambini
kisiwani Zanzibar, inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya
taifa ya Wanawake kutoka Kenya (Harambee Starlets) Agosti 23, 2015.
Mchezo
huo wa kirafiki utachezwa katika uwanja wa Aman Kisiwani Zanzibar,
ikiwa ni sehmu ya maandalizi ya kikosi hicho kujiandaa na fainali za
Michezo ya Afrika (All Africa Games) zitakazofayika nchini
Congo-Brazzavile kuanzia Septemba 4 – 19, 2015.
Twiga
Stars inaendelea na mazoezi kutwa mara mbili katika viwanja vya Aman na
Fuoni chini ya kocha wake mkuu Rogasian Kaijage kujiandaa na fainali
hizo za michezo ya afrika, wachezaji wote waliopo kambini wapo katika
hali nzuri wakiendelea kujifua na michezo ya Afrika.
USAJILI Dirisha
la usajili limeongezwa toka tarehe 06 Agosti hadi tarehe 20 Septemba,
baada ya muda huo klabu itakayochelewesha kuleta usajili wake itatozwa
kiasi cha shilingi laki tano (Tsh 500,000) kwa kila mchezaji
itakayemsajili mpaka siku ya tarehe 30 Agosti.
Mwisho wa kufanya uhamisho wa kimataifa wa wachezaji kwa njia ya mtandao TMS ni tarehe 6 Septemba.
Kikao
cha kamati ya sheria kitakaa tarehe 28 kwa ajili ya kuupitisha usajili
na kitakaa tena tarehe 8/9/2015 kwa ajili ya kupitisha usajili.
Kuanzia
tarehe 21 hadi 27 itakuwa ni wiki ya pingamizi, ambapo majina
yatabandikwa TFF Karume na kuwekwa kwenye mtandao ili kuwezesha vilabu
vyenye pingamizi kuwawekea wachezaji mapingamizi.
Ligi
Kuu ya Vodacom (VPL) inatarajiwa kuanza tarehe 12 Septemba 2015, Daraja
la kwanza (FDL) ikitarajiwa kuanza Septemba 17 na Ligi Daraja la pili
inatarajiwa kuanza Oktoba 16 mwaka huu.
MICHUANO YA COPA COCA-COLA 2015
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) bado linaendelea na mazungumzo na
wadhamini wa michuano hiyo (Coca-Cola). Kutokana na mazungumzo
hayo, ratiba ya michuano hiyo itachelewa kutoka.
Hivyo, tunawaomba kuwa na uvumilivu wakati mchakato wa mazungumzo hayo yanayokaribia ukingoni ukiendelea.
0 comments :
Post a Comment