BASI LA NEW FORCE KUTOKA DAR KWENDA TUNDUMA LAUA 12 NA KUJERUHI 28 BAADA YA KUGONGWA NA ROLI MKOANI IRINGA

fo1
Inasadikika watu 12  wamepoteza Maisha na wengine  28 wamejeruhiwa jana baada ya basi la New Force kupata ajali Eneo la Mahenge Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa barabara kuu ya Iringa- Dar es salaam
Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo,Kamanda wa polisi MKOA wa IRINGA Peter kakamba amesema kuwa basi la kampuni ya New Force  lenye namba za usajili T483 CTF lililokuwa ikitokea Dar es Salaam kwenda Tunduma limepata ajali eneo la MAHENGE kwa kugongana na Roli  aina ya Scania lililokuwa limebeba mbao likitokea NJOMBE kwenda Dar es Salaam .
Amesema kuwa ajali hiyo imesababishwa na kupasuka kwa tairi la MBELE la loli,na baadae likakosa mwelekeo ndipo lilienda kugonga basi hilo na kuuwa watu 12 na kujeruhi 28.
Kamanda Kakamba Amesema kuwa maiti zimehifadhiwa katika hospital ya MKOA wa IRINGA,na majeruhi wanaendelea kupata matibabu.
Kwa upande wa mganga MKUU mfawidhi wa hospital ya MKOA wa IRINGA Dkt Mseleta Nyakiroto amethibitisha kupokea maiti na majeruhi katika hospital hiyo na kusema kuwa majira ya SAA tisa na nusu jana alipewa taarifa ya kutokea kwa ajali na taratibu za kupokea majeruhi na maiti zikafuata.
Aidha mganga huyo amesema kuwa maiti zote bado  
hazijatambuliwa   na ndugu zao.
fo2
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment