Serikali Yabanwa ....Yakubaliana na Hoja ya Wapinzani......Yauondoa Mpango wa Maendeleo ya Miaka Mitano Bungeni

Nkupamah media


Serikali imeamua kuondoa hoja yake ya mpango wa maendeleo wa miaka mitano iliyokuwa imeuawasilisha mapema leo bungeni baada ya kudaiwa kuwa kilichowasilishwa hakikuwa mpango wa miaka mitano bali mwelekeo wa mpango wa mwaka mmoja.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya wabunge Tundu Lissu na Zitto Kabwe kupinga mjadala wa hoja hiyo katika kikao cha leo mchana kuwa hakuna haja ya kuendelea na mjadala hadi serikali ipeleke mpango wa miaka mitano ukiambatana na muswada wa sheria husika.

Katika kikao hicho, ilipelekea mwenyekiti wa bunge Andrew Chenge kuahirisha kikao baada ya kambi ya upinzani kugoma kutoa maoni yake kupitia kwa mbunge David Silinde, na kupangwa kikao hicho kingeendelea jioni.

Katika kikao cha jioni, Mwenyekiti wa bunge alilazimika kuahirisha bunge hadi Jumatatu ijayo baada serikali kukubali kuondoa hoja yake kwa ajili ya kujipanga upya.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment