KPMG YAWA KINARA KUNDI LAO KATIKA MICHUANO YA AWESOME BONANZA 2016

Nkupamah media:

Kikosi cha timu ya KPMG  Waliosimama kutoka kushoto ni
Isyaka,Bakari,Isaya, Nsanyiwa,Hamza(kocha),Getrude(kiongozi wa timu) na
Jovin.  Walioinama kutoka kushoto ni  Evans, Denis, Jamal, Thobias, Frank, Ahmed na Amiri.    Aliyelala ni Jim aka Messi wa
KPMG katika michuano ya Awesome Bonanza mwishoni wa wiki iliyopita ambapo
michuano hiyo imeandaliwa na Jarida la kila mwezi la Awesome magazine

 Kikosi cha wachezaji wa Kampuni ya KPMG katika picha ya pamoja katika michuano ya Awesome Bonanza mwishoni wa wiki iliyopita ambapo michuano hiyo imeandaliwa na Jarida la kila mwezi la Awesome magazine

 Wachezaji wa timu ya KPMG wakiwa mapumziko kutoka kushoto walioangalia mbele Bakari , Dennis, hamza (kocha mchezaji) na isyaka katika michuano ya Awesome Bonanza mwishoni wa wiki iliyopita ambapo michuano hiyo imeandaliwa na Jarida la kila mwezi la Awesome magazine

Wachezaji wa timu ya KPMG wakishangilia Goli dhidi ya Timu ya Deloitte katika michuano ya Awesome Bonanza mwishoni wa wiki iliyopita ambapo michuano hiyo imeandaliwa na Jarida la kila mwezi la Awesome magazine

Wachezaji wa KPMG wakishangilia Goli lilifungwa na mshambuliaji wao machachari Daudi Mbaga dhidi ya  timu ya PWC katika michuano ya Awesome Bonanza mwishoni wa wiki iliyopita ambapo michuano hiyo imeandaliwa na Jarida la kila mwezi la Awesome magazine

 Kiungo wa Timu ya KPMG Bakari Mkupe akiwania mpira na wachezaji wa Timu ya PWC.katika michuano ya Awesome Bonanza mwishoni wa wiki iliyopita ambapo michuano hiyo imeandaliwa na Jarida la kila mwezi la Awesome magazine
Wafanyakazi  wa kampuni ya KPMG waliokuja kushangilia wenzao  kutoka kushoto ni Asha, Mumtaz,Lilian, Witness, Getrude, patricia, desire na Grace.katika michuano ya Awesome Bonanza mwishoni wa wiki iliyopita imeandaliwa na Jarida la kila mwezi la Awesome
magazine

………………………………………………………………
                                     Na Krantz Mwantepele,Dar es salaam                                                                                              
Timu ya mpira wa miguu ya kampuni ya uhasibu ya KPMG ilishiriki michuano ya Awesome Bonanza siku ya
Jumamosi tarehe 6-Feb 2016 na kuibuka kinara katika kundi lao lililohusisha
timu nyingine za makampuni yanayohusika na uhasibu pia.
 Michuano hiyo ambayo imeandaliwa na Jarida la
kila mwezi la Awesome magazine ilianza siku ya jumamosi tarehe 6 feb 2016
ikifanyika katika viwanja vya Jakaya Kikwete Park vilivyopo maeneo ya Mnazi
Mmoja zamani kidongo chekundu kwa hatua za Makundi kwa kundi la timu kutoka
kampuni  za uhasibu.
Katika kundi hilo zilikuwepo timu kutoka kampuni za uhasibu za Deloitte, PWC na Innovex.
Timu ya kampuni ya  KPMG iliibuka kinara wa kundi hilo kwa kupata
ushindi katika mechi zao zote. KPMG ilipata matokeo yafuatayo: KPMG 3-1 PWC,
KPMG 4-1 Deloitte , KPMG 2-1 Innovex. Hivyo kuwafanya wasonge mbele katika
micuano hiyo itakayoendelea mwezi huu.
Wafungaji wa magoli ya
KPMG walikuwa
Jim Mwasigala (3)
Bakari Mkupe (2)
Frank Mboya (2)
Ahmed Mohammed
Daudi Mbaga
Akiongea baada ya mechi
hizo kocha mchezaji wa timu ya KPMG, Hamza Mzee amesema ya kwamba timu kampuni
ya KPMG imejiandaa vyema na wana uhakika wa kushinda michuano hiyo kwa kuwa
wanajali utamaduni wa kufanya mazoezi kupitia michezo kwa kuwa huboresha Afya
kwa ujumla.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment