NANDY KUPEPERUSHA BENDERA YA TANZANIA HUKO NIGERIA KATIKA TECNO ONW THE STAGE GRAND FINALE

Nkupamah Media:


    Msanii Faustina Charles Mfinanga ambaye akiwa nyumbani kwao kwa baba na mama huitwa Nandela ataiwakilisha Tanzania ktk mashindano ya fainali ya Tecno onw the stage yatakayo fikia tamati yake February 7 mwaka huu huko Nigeria.
      Mwana dada huyo ambaye jina lake la kisanii anaitwa Nandy na limetokana na jina lake la Nandela.Alishiriki kwa mara ya kwanza mnamo mwezi October 2015 katika Hotel moja hapa Dar es salaam ambapo walikuwa wakisakwa wasanii watano watakao iwakilisha Tanzania nchini Nigeria.Katika hatua hii kulikuwa na wasanii zaidi ya 50 na akafanikiwa kutinga tano bora.Wengine waliotinga tano bora ni pamoja na Zuchu,Kechu,Banye na Kandi Jefu.
       Mashindano haya yanashirikisha nchi 3 yaani Kenya,Tanzania na wenyeji Nigeria,ambapo katika hatua 12 za mchujo Zechu,Kechu,Banye na Jefu toka Tanzania wamotolewa ktk mashindano,pia katika hatua hiyo ya fainali Wakenya 2 na Mnaigeria mmoja wamebakia ktk fainali hiyo,huku Tanzania ikiwakilishwa na msanii  Faustina Charles a.k.a Nandy ambapo amekwea pipa leo kuelekea nchini Nigeria.Kila lakheri Nandy katika fainali hizo Watanzania wapo nyuma yako.Kumpigia kura Nandy nenda kwenye tovuti hii http://tecnoownthestage.com/vote/

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment