JERRY MURO HANA KESI YA KUJIBU, AACHIWA AENDE ZAKE



Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imetupilia mbali shauri la Msemaji wa Yanga, Jerry Muro kusikilizwa.

Kamati hiyo imesema hoja zilizotolewa ili kumuita Muro zilikuwa na mapungufu na haikuona kama kuna sababu ya kumuita na kumhoji.

“Kweli kamati ya maadili imetupilia mbali, ninaona ni ushindi kwa Wanayanga na ninawasamehe wote walionitesa.

“Huu ni ushindi wa Wanayanga wote, lakini wito wangu kwa sasa ni sote kuungana, kwa Wanayanga na TFF kwa ajili ya maendeleo ya soka nchini,” alisema Muro katika ujumbe wake mfupi.


Jerry aliitwa kwenye kamati ya maadili baada ya TFF kupitia katibu wake mkuu, Mwesigwa Celestine kumtumia barua hiyo ya wito ingawa nayo ilikuwa na mpungufu rundo kwani haikueleza hata anatakiwa katika kamati ipi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment