Bodi
ya Wadhamini ya Chama cha Wananchi (CUF) leo imefungua kesi namba 23 ya
mwaka 2016 katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, dhidi ya Msajili
wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, Mwanasheria Mkuu wa
Serikali,George Mcheche Masaju, Profesa Ibrahim Lipumba pamoja na
waliokuwa wanachama wa chama hicho wapatao 11.
Wakili
wa Mahakama Kuu na Mwanasheria wa CUF, Hashimu Bakari Mzirai wakati
akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufungua kesi hiyo, amesema
Bodi ya Wadhamini ya CUF imeifungua kesi hiyo kwa hati ya dharula kwa
lengo la kusikilizwa kwa haraka ili mahakama itoe maamuzi mapema.
“Kuhusiana
na kesi tuliyoahidi watanzania kuwa chama kinaenda kuifungua dhidi ya
msajili wa vyama vya siasa, mwanasheria mkuu wa serikali, Lipumba na
wanachama waliokiasi chama,” amesema.
Ameongeza kuwa “Kesi hii
imefunguliwa leo na jopo la mawalili wa CUF, imeletwa kwa hati ya
dharula, imesajiliwa na tutawapa maelezo zaidi hapo baadae sababu kesi
itapangwa kwa jaji muda si mrefu,”
Mziray
amedai kuwa, katika kesi hiyo, bodi imeiomba mahakama kuu mambo matatu,
kwanza kutengua barua ya Septemba 23, 2016 kutoka kwa Jaji Mutungi
aliyodai kuwa ililenga kutengua maamuzi halali ya vikao vya chama hicho
kutokana kwamba barua hiyo ilieleza kuwa ofisi ya msajili wa vyama vya
siasa inamtambua Prof. Lipumba kama mwenyekiti wa chama hicho.
Pili,
kumzuia Msajili wa Vyama vya Siasa kuingilia maamuzi ya chama hicho ya
kumfuta uanachama Lipumba kwa madai kuwa chama hicho kupitia Baraza Kuu
la Uongozi kimemfuta uanachama.
Jambo
la mwisho, Mziray amedai kuwa, bodi hiyo pamoja na viongozi wa CUF,
inataka kufanya siasa na kwamba inaona msajili ndiyo kikwazo cha
shughuli zake hususan za kisiasa za chama hicho ambapo imeitaka mahakama
imzuie kuingilia masuala ya CUF na kuingilia maamuzi ya vikao halali
vya chama.
Mziray
ameeleza kuwa “Hati ya darura hutoeka pale kunapokuwa na jambo la
hatari nadhani mnafahamu kwamba ofisi kuu ya chama imeshimiliwa na watu,
na kwamba imefungua kesi kwa hati ya dharula ili iweze kudhibiti ofisi
zake hasa ofisi kuu iliyopo buguruni.Jambo la pili wanachama wanashauku
ya kujua hatma ya chama chao nashukuru kwamba mahakama ina spidi ya
kusikiliza kesi hivyo wanachama watafahamu hatma ya chama chao hivi
karibuni,”
0 comments :
Post a Comment