Mahakama Yamfutia Shtaka la Unyang’anyi wa Kutumia Silaha Scorpion




Salum Njwete maarufu kama ‘Scorpion’ anayetuhumiwa kumchoma kisu na kumtoboa macho, Saidi Mrisho amefikishwa mahakama ya Ilala Dar es salaam leo na kusomewa shitaka la unyang’anyi kwa kutumia silaha.
Upande mashitaka uliiomba mahakama kuliondoa shitaka la unyanganyi wa kutumia silaha linalomkabili Salumu Njwete kwa nia ya kutotaka kuendelea nalo.
Kutokana na ombi hilo hakimu Adelf Sachole alikubaliana na ombi hilo kuliondoa shitaka hilo kupitia kifungu cha 91 (1) ambapo kinampa mamlaka mkurugenzi wa mashitaka (DPP) kuondoa mashitaka muda wowote ilimradi isifike kwenye hukumu.
Baada ya saa kadhaa alifunguliwa shitaka hilohilo tena  la unyang’anyi kwa kutumia silaha alilolifanya September 6 2016  Buguruni sheli Dar es salaam na jumla ya vitu alivyochukua 476000 kwa hakimu mwengine Frola Haule. Salumu alikana mashitaka hayo.
Kutokana na kesi inayomkabili kisheria haina dhamana amerudishwa rumamde na kesi hiyo itatajwa tena November 2 2016
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment