Mwezi
mmoja baada nahodha wa zamani wa Barcelona, Xavi Hernandez kupishana
maneno na Cristiano Ronaldo baada ya Ronaldo kusema hawezi
kujilinganisha na Messi, mkongwe huyo amezungumzia nafasi ya Ronaldo
kushinda tuzo ya Ballon d’Or.
Xavi
amesema kwa uwezo ambao anaonyesha kwa sasa Ronaldo anaamini staa huyo
wa Real Madrid ana nafasi ya kushinda tuzo hiyo kutokana na mafanikio
aliyoyapata kwa mwaka huu.
“Cristiano
ana namba ya kushinda Ballon d’Or mwaka huu, ameshinda Ligi ya Mabingwa
na Kombe la Euro akiwa na Real Madrid na Ureno,
“Lakini nafikiri jambo hilo litakuwa na ushindani mkubwa, kwasababu hata Messi yupo,” alisema Xavi.


0 comments :
Post a Comment