JK: Sikuidhalilisha Tume ya Warioba

Kwa ufupi
Alifafanua kuwa hotuba yake ililenga kuwashauri wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kuangalia kwa kina masuala yaliyomo ndani ya Katiba ili kufanya uamuzi sahihi.


Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete amesema kuwa hakuwa na nia ya kuidhalilisha Tume ya Mabadiliko ya Katiba wakati alipohutubia kulifungua Bunge Maalumu la Katiba, wiki mbili zilizopita.
Rais Kikwete alisema hayo jana kwenye ziara yake ya siku tatu ya kidola nchini Uingereza, moja ya ziara nadra kufanywa na viongozi wa nchi za nje nchini humo.
Alisema kuwa anawaheshimu sana wazee waliokuwa wanashughulikia mchakato mzima wa kuandaa Rasimu ya Katiba Mpya, hivyo hakukuwa na sababu ya yeye kuwafanyia jambo hilo.
“Watu wamesema eeeh! umeidhalilisha tume!… Siwezi kufanya kazi hiyo! Nawaheshimu sana hao wazee ndio walionilea mpaka hapa nilipofika,” alisema Kikwete.
Alifafanua kuwa hotuba yake ililenga kuwashauri wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kuangalia kwa kina masuala yaliyomo ndani ya Katiba ili kufanya uamuzi sahihi.
Wakati akiwasilisha hotuba yake bungeni hivi karibuni, Rais alionekana kutilia shaka takwimu zilizotolewa na tume hiyo.
“Nilitoa maoni yangu ya rasimu kwa sababu ninayo dhamana hiyo… Wao walitaka niseme; wajumbe nimelizindua Bunge. Hiyo haiwezekani,” aliongeza Rais Kikwete akiashiria kuwa
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment