Kwa ufupi
Dar es Salaam. Rais Jakaya 
Kikwete amesema kuwa hakuwa na nia ya kuidhalilisha Tume ya Mabadiliko 
ya Katiba wakati alipohutubia kulifungua Bunge Maalumu la Katiba, wiki 
mbili zilizopita.
Rais Kikwete alisema hayo jana kwenye ziara yake 
ya siku tatu ya kidola nchini Uingereza, moja ya ziara nadra kufanywa na
 viongozi wa nchi za nje nchini humo.
Alisema kuwa anawaheshimu sana wazee waliokuwa 
wanashughulikia mchakato mzima wa kuandaa Rasimu ya Katiba Mpya, hivyo 
hakukuwa na sababu ya yeye kuwafanyia jambo hilo.
“Watu wamesema eeeh! umeidhalilisha tume!… Siwezi 
kufanya kazi hiyo! Nawaheshimu sana hao wazee ndio walionilea mpaka hapa
 nilipofika,” alisema Kikwete.
Alifafanua kuwa hotuba yake ililenga kuwashauri 
wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kuangalia kwa kina masuala yaliyomo 
ndani ya Katiba ili kufanya uamuzi sahihi.
Wakati akiwasilisha hotuba yake bungeni hivi karibuni, Rais alionekana kutilia shaka takwimu zilizotolewa na tume hiyo.
“Nilitoa maoni yangu ya rasimu kwa sababu ninayo 
dhamana hiyo… Wao walitaka niseme; wajumbe nimelizindua Bunge. Hiyo 
haiwezekani,” aliongeza Rais Kikwete akiashiria kuwa 

0 comments :
Post a Comment