Shambulizi lawaua watu 4 Burundi

Polisi nchini Burundi wanasema kuwa watu wanne wameuawa na wengine karibu 30 kujeruhiwa kwenye mashambulizi ya guruneti Jumapili usiku.
Mashambulizi hayo yalifanyika katika miji mitatu ukiwemo mji mkuu Bujumbura.
Polisi wanasema kuwa guruneti hizo zilirushwa na wafuasi wa upinzani ambao wanataka kuvuruga uchaguzi mkuu unaokuja.
Siku ya ijumaa watu 11 walijeruhiwa kwenye misururu ya mashambulizi ya guruneti.
Burundi imekumbwa na ghasia zilizoendeshwa na wapinzani wa rais Nkurunziza wanaopinga uamuzi wake wa kugombea urais kwa muhula wa tatu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment