Fastjet kuanza ‘route ya 5’ leo ni ya Dar- Lilongwe (Malawi)


DSC_0480.jpghhhMeneja Mkuu wa shirika la Ndege la Fastjet Afrika Mashariki, Jimmy Kibati akifafanua jambo kwa waandishi (hawapo pichani) wakati wa mkutano maalum na wanahabari akielezea namna fastjet inavyotanua safari zake katika nchi za Afrika, mkutano uliofanyika hivi karibuni Unguja-Zanzibar wakati wa tamasha la 18, la filamu za nchi za majahazi maarufu ZIFF, ambapo fastjet pia ni wadhamini kwa miaka miwili mfululizo (Picha na Andrew Chale wa modewjiblog).

Na Andrew Chale, modewjiblog
(Dar Es Salaam) Shirika la ndege la Fastjet  limeendelea kupanua wigo wake kwa kuanzisha safari zaidi ikiwa ni kuunganisha Afrika kuwa moja kupitia safari za anga kwa gharama nafuu kabisa ambapo asubuhi ya leo  wanatarajia kuizindua rasmi ‘route’ hiyo ambayo inakuwa ni ya tano ya kutoka Dar es Salaam-Tanznaia kwenda Lilongwe-Malawi.
Awali akielezea kwa wandishi wa habari, Meneja Mkuu wa shirika la Ndege la Fastjet Afrika Mashariki, Jimmy Kibati alipokutana Zanzibar wakati wa tamasha la 18, la filamu za nchi za Majahazi maarufu ZIFF ambapo pia Fastjet ni wa zamani kwa mwaka wa pili mfululizo, alibainisha kuwa maar azote shirika hilo linakuja na huduma bora na kwa gharama nafuu kumsaidia mteja kufanikisha mambo yake mbalimbali kupitia usafiri wa anga.
Anasema kuanzishwa kwa ‘route’ hiyo ya Lilongwe (Malawi), fastjet ipo  pia mbioni kufikia nchi zingine ndani ya Afrika na kwa sasa ipo katika mchakato huo na baadae wataweza kutangaza rasmi huku akiwataka wateja kujitokeza kwa wingi kuwaunga mkono katika juhudi hizo za usafirishaji wa anga.
“Tunajisikia furaha kuweza kusogeza huduma zaidi wateja waliokuwa wakitumia muda mrefu kusafiri kutumia usafiri mwingine kuelekea Malawi, sasa wamepata mkombozi Fastjet ambayo itakuwa ikiruka mara mbili kwa wiki Jumatatu na Ijumaa!… kwa gharama nafuu kabisa” alieleza Kibati.
Kwa upande wake, Afisa Mahusiano na Masoko wa Fastjet, Lucy Mbogoro  anasema tayari watu mbalimbali wameweza kuchangamkia ‘route’ hiyo ya kuelekea Malawi kwani itaendelea kuunganisha watu wote karibu huku ikitoa fursa kwa wafanyabiashara, wanafunzi, shughuli za kiserikali, michezo pamoja na zingine nyingi ikiwemo za kifamilia.
Awali Fastjet ilianzia na safari za ndani za kusafirisha abiria ‘route’ za Mwanza – Dar, Kilimanjaro – Dar na Mbeya – Dar na baadae kuweza kuvuka mipaka zaidi kwa nchi za Afrika kwa ‘rout’ kati ya Dar – Johannesburg (Afrika Kusini), Dar – Lusaka (Zambia), Dar – Harare (Zimbabwe), Dar – Entebbe (Uganda) na kwa sasa hii inayozinduliwa leo Julai 27, ya Dar-Lilongwe (Malawi).
Afisa huyo, anaeleza kuwa, Fastjet itaendelea kutoa huduma bora kupitia usafiri wa anga huku akisisitiza kuwa ‘route’ mbalimbali zikiwa mbioni kufikiwa na shirika hilo.

Want to take your business to Malawi’s thriving capital city?ggNow you can. Our new international route connects Lilongwe with Dar es Salaam every Monday and Friday with fares available from just Tsh 237,600/$99 (Tsh 120,000/$50 fare, plus Tsh 117,600 tax/$49 gov.taxes).

Tickets are on sale now with flights departing from 27th July, so save yourself the hassle of a long drive and fly further for less with fastjet.com
bMeneja Mkuu wa shirika la Ndege la Fastjet Afrika Mashariki, Jimmy Kibati katika mahojiano na wanahabari..
kibatiMeneja Mkuu wa shirika la Ndege la Fastjet Afrika Mashariki, Jimmy Kibati akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati wa mkutano huo..
fastjetMuonekano wa moja ya  ndege za fastjet kwa ndani…
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment