Mkurugenzi
wa Bushback Safaris Mustafa Panju ambaye ni mtia nia ubunge wa jimbo la
Arusha kwa tiketi ya CCM akinadi sera zake mbele ya wanachama wa chama
hicho katika kata ya ungalimited jijini Arusha ili kuomba ridhaa ya
kuteuliwa kuwamgombea wa ubunge jimbo la Arusha kupitia CCM ambapo
aliwataka wananchi hao kuchagua kiongozi sahihi wakuweza kuleta
mabadiliko katika jimbo la Arusha pia alisema yupo tayari kushirikiana
na mgombea atakayepitishwa na chama hicho endapo chama hicho hakitamteua
kuwa mgombea Ubunge jimbo la Arusha mjini.
Habari picha na Pamela Mollel wa jamiiblog
Katibu
wa CCM wilaya ya Arusha, Ferooz Bano ambaye pia ni msimamizi wa
uchaguzi akitoa maelekezo kwa wananchi wa kata ya Ungalimited namna ya
kuwasikiliza wagombea ambapo aliwataka wasipige makofi wala kushangilia
wakati wagombea hao wakijinadi kwa sera zao
Wagombea 12 ubunge kwa tiketi ya chama cha mapinduzi wakiwa katika kata ya Ungalimited mtaa wa Esso
Taswira
mama akiwa amembeba mwanae akiwa anavuka barabara wakati mkutano wa
kujinadi wagombea wa chama cha mapinduzi ukiwa unaendelea katika kata ya
Ungalimited mtaa wa Esso jijini hapa
Kulia
ni Mkurugenzi wa Bushback Safaris Mustafa Panju ambaye ni mtia nia ya
ubunge wa jimbo la Arusha kwa tiketi ya CCM akifwatilia sera za wagombea
Ubunge mbele ya wanachama wa chama hicho katika kata ya ungalimited
jijini Arusha.
Wanachama
na wananchi waliojitokeza kuwasikiliza watia nia nafasi ya Ubunge jimbo
la Arusha mjini kupitia chama cha mapinduzi CCM
Sehemu ya akinamama wakereketwa wa chama cha mapinduzi.
Mkurugenzi
wa Bushback Safaris Mustafa Panju ambaye ni mtia nia ya ubunge wa jimbo
la Arusha kwa tiketi ya CCM akinadi sera zake mbele ya wanachama wa
chama hicho katika kata ya ungalimited jijini Arusha ili kuomba ridhaa
ya kuteuliwa kuwamgombea wa ubunge jimbo la Arusha kupitia CCM ambapo
aliwataka wananchi hao kukipenda chama huku akiomba ridhaa ya
kuwatumikia endapo atapita katika kura ya maoni
Mwanadada
mlemavu akiwa anasikiliza kwa umakini sera za wagombea ubunge kupitia
chama cha mapinduzi CCM katika kata ya Sekei uwanja wa Tax sanawari.
Mkurugenzi
wa Bushback Safaris Mustafa Panju ambaye ni mtia nia ya ubunge wa jimbo
la Arusha kwa tiketi ya CCM akiwa anasikiliza sera za wagombea wenzake
katika kata ya sekei jijini Arusha ambapo alisema kuwa endapo chama
hicho hakitampitisha yupo tayari kushirikiana na atakayepitishwa na
chama hicho.
Taswira picha mbalimbali za wagombea ubunge CCM zikipamba ukuta katika eneo la sanawari
Mkusanyiko mkubwa wa watu wakitawanyika baada ya mkutano wa wagombea ubunge kuisha katika kata ya kaloleni jijini Arusha.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 comments :
Post a Comment