RAIS WA FFB KUWASILI LEO

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Burundidownload (7) (FFB), Reverien Ndikuriyo anatarajiwa kuwasili leo saa 5 usiku jijini Dar es salaam kwa shirika la Ndege la Rwanda Air.
Ndikuriyo anatarjaiwa kuwa na mazungumzo na Rais wa TFF, Jamali Malinzi kisha atashuhudia michuano ya kombe la Kagame inayoendelea kutimua vumbi jijini Dar es salaam ikiwa katika hatua ya robo fainali kwa sasa.
Aidha Vicent Nzamwita Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Rwanda (FERWAFA) anatarajiwa kuwasili nchini alhamis akiambatana na kocha wa timu ya Taifa ya Rwanda (Amavubi) John McKinstry.
Rais wa FERWAFA anatarajiwa kuwa na mazungumzo na Rais wa TFF, Jamal Malinzi na baadae kuhudhuria michuano ya Kombe la Kagame inayoendelea nchini Tanzania
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment