Waziri
wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Saada Mkuya Salum
akizungumza katika siku ya pili ya mkutano wa tatu wa kimataifa kuhusu
ufadhili wa maendeleo ( FFD3) unaoendelea jijini Addis Ababa- Ethiopia
Na Mwandishi
Maalum,
New York
Mkutano wa tatu wa
kimataifa kuhusu ufadhili wa maendeleo,
( FFD3) jana (jumanne) umeingia siku yake
pili ambapo Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mhe. Saada Mkuya
Salum alielezea matumaini ya Tanzania
juu ya matokeo ya mkutano huo katika kusukuma mbele ajenda ya maendeleo
endelevu.
Waziri wa Fedha ambaye anamwakilishi Mhe. Rais Jayaka Mrisho Kikwete katika mkutano
huo, amesema kuwa, Tanzania
inaamini kwamba ufadhili wa maendeleo ni moja ya ajenda muhimu kwa Bara
la Afrika . Kwa sababu hiyo Tanzania, inategemea
kuona ufadhili huo unakuwa
na matokeo makubwa katika
kuondoa umaskini katika nchi nyingi za
Afrika.
“ Kama kweli
tunataka kuwa na utekelezaji wa uhakika wa malengo ya maendeleo endelevu baada ya 2015,
Matumaini ya nchi yangu ni kuona kuwa
mkutano huu unatoka na matarajio
mathubuti yatakayo hakikisha mtiririko usio shaka wa rasilimali kuchagiza maendeleo”. Amesema
Mhe.Waziri
Ametoa wito wakuwapo kwa mikakati ya
pamoja baina ya pande zote, kule zitokako au asili ya
raslimali hizo na nchi zinazopokea misaada hiyo lengo likiwa kudhibiti
mrititiko wa fedha chafu, uwezeshwaji wa kukomboa raslimali na
kuzirejesha raslimali hizo kwa nchi husika.
“ Afrika inapoteza karibu
dola bilioni 50 kwa mwaka
kutokana na mtiririko wa fedha chafu
kutoka nchi zinazoendelea, hali
inayosababisha kusababisha uhaba mkubwa
wa hazina ya fedha za kigeni, kupungua kwa makusanyo ya kodi, kufutwa
vyanzo vya uwekezaji uwekezaji na hatimaye kuongezeka kwa umaskini”.
Amesema Waziri wa Fedha.
Kiongozi huyo wa ujumbe wa
Tanzania katika mkutano huo, ameelezea
umuhimu wa Mkakati wa Addis Ababa kujielekeza na kuwa mfumo
madhubuti utakaoimarisha ushirikiano katika masuala ya kodi.
Vile
vile Waziri wa fedha, amesisitiza kwamba takwimu zitakazotumiwa na
Taasisi ambazo zitapewa jukumu la kufuatilia na kufanya marejeo
kuhusu ufadhili wa maendeleo , takwimu hizo ni lazime zitoke
katika taasisi za takwimu ambazo
zinatambuliwa na serikali ya nchi husika.
Akabinisha
kwamba matumizi ya takwimu
rasmi kutoka taasisi
zinazotambuliwa na serikali , kutaepusha
kutumiwa kwa takwimu ambazo si rasmi na hivyo kusababisha
sitofahamu na migongano kati ya
Nchi wanachama na Umoja wa
Mataifa.
Waziri
Saada Mkuya Salumu akatoa wito wa kuongezwa raslimali fedha
hususani kwa nchi zinazoendelea ili ziwe na uwezo wa kuboresha
mifumo yake ya
ukusanyaji wa takwimu, kuzichambua na kuzifanyia tathmini.
MONUSCO YAHITAJI USHIRIKIANO WA KARIBU ZAIDI NA DRC
Na Mwandishi Maalum, New York
Uwezo wa Misheni ya
Ulinzi wa Amani katika Jamhuri
ya Kidemokrasia ya Kongo ( MONUSCO) wa
kutekeleza mamlaka yake kikamilifu utategemea zaidi ushirikiano na uhusiwano wake na mamlaka
za nchi hiyo.
Hayo yameelezwa na Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa
Mataifa katika DRC, Bw. Martin Kobler wakati alipowasilisha taarifa yake
mbele ya wajumbe wa Baraza Kuu
la Usalama la Umoja wa Mataifa siku ya jumaane.
Taarifa Bw. Kobler
kwa Baraza hilo ilihusu maeneo matatu
ambayo ni uchaguzi mkuu utaotarajiwa
kufanyika mwakani, hali ya
usalama na mkakati wa upunguzaji wa idadi ya walinzi wa Amani.
“
Mafanikio ya utekelezaji wa mamlaka yetu
unategemea na kuendelea kwa majadiliano
na ushirikiano na serikali na hususanu kuhusu hali
ya usalama katika eneo la Mashariki na
Mchakato wa Uchaguzi.
Akielezea zaidi kuhusu hali ya usalama,
Mwakilishi wa Katibu Mkuu, ameliambia
Baraza kwamba, kuna matumaini
katika baadhi ya maeneo.
Akibainisha juu ya operesheni
zinazoendelea dhidi ya kundi la
wanamgambo la Force
de Resistance Patriotique en Ituri ( FPRI) na zinazofanywa na
Jeshi la DRC ( FARDC) kwa kusaidiwa na MONUSCO.
“
Wakati kipaumbele ni kuhakikisha kuwa kundi
hili linasalimisha silaha kwa
hiari, matumizi ya nguvu ilibidi
yafanyike baada ya kunvujwa mara tatu
muda wa mwisho ambao kundi hilo
lilipashwa kusalimisha silaha
zake kwa hiari” amesema Bw. Kobler
Kuhusu operesheni ya pamoja
dhidi ya kundi la Force Democratique de
Liberation du Rwanda ( FDLR) katika
maeneo ya Kivu Magharibu, Kivu ya Kusini na Katanda amsema operesheni hiyo imesimama kwa zaidi ya miezi mitano.
Amefafanua kuwa kusimama kwa
operesheni hiyo ambayo ilitakiwa
ifanywe na FARDC kwa kusaidiwa na
MONUSCO licha ya kwamba pamoja na mambo mengine kulitoka na hoja ya
awali kuhusu haki za binadamu
bali sasa limekwenda mbali zaidi ya hapo.
Akaongeza kwamba wakati MONUSCO ikirejea na kufanya tathmini kuhusu
haki za binadamu ilikuwa inatafuta njia ya namna ya kuendeleza ushirikiano
kupitia mpango uliopo sasa.
Akielezea zaidi kuhusu hali ya
usalama, Bw. Martin Kobler amesisitiza
kuwa wakati serikali ya DRC imepiga hatua kubwa katika kurejesha hali ya Amani katika baadhi ya maeneo ya nchi hiyo. Bado
wananchi wa eneo la Mashariki ya
nchi hiyo maisha yao yanategemea sana huruma ya makundi ya wanamgambo
wenye silaha.
Pamoja na
mafanikio ya kupunguza
nguvu ya FDLR katika baadhi ya maeneo waliyokuwa wakiyakalia, jeshi la DRC
limejikuta katika mazingira magumu
ya kuyadhibiti na kuyashikilia maeneo yaliyokombolewa na
kwamba hakuna muda wa kusubiri.
Kuhusu uchanguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Novemba
mwaka 2016, Bw. Kobler amesema wajibu wa kuhakikisha kwamba uchaguzi huo
unakuwa wa huru, haki na wazi ni wa serikali yenyewe ya DRC
Akaongeza
kwamba tajio
la haraka katika kuhakikisha
kwamba uchaguzi utafanyika kwa wakati ni fedha , kalenda sahihi ya
uchaguzi,
uboreshaji wa daftari la wapiga kura na utoaji wa fursa kwa vyama vya
upinzani. Akamsifu Rais Kabila kwa kupanua wigo wa majadiliano
na wadau mbalimbali katika kipindi cha kuelekea uchaguzi.
Katika hatua nyingine. Mwakilishi wa Jordan na ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Vikwanzo dhidi ya DRC, Dina Kawar ,
ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kwa kumkamata na kisha
kukubali kumpeleka nchini Uganda kiongozi wa Kundi la Allied Democratic Force ( ADF) Bw. Jamil
Mukulu
Ametoa shukrani hizo wakati naye alipokuwa akiwasilisha taarifa ya Kamati yake mbele ya Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa


0 comments :
Post a Comment