UPENDO NKONE KUMSINDIKIZA BONNY MWAITEGE

MWIMBAJI nguli wa muziki wa Injili Tanzania, Upendo Nkone amekuwa wa kwanza kujitokeza kusindikiza uzinduzi wa mwenzake Bonny Mwaitege, utakaofanyika Agosti 2 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama Nkone amekuwa wa kwanza na ameonesha nia ya kumsindikiza Mwaitege kwa sababu ya ubora wa uzinduzi huo. “Uzinduzi wa Mwaitege utakuwa ni wa aina yake kwa sababu maandalizi yake kwa yamefanywa kwa ustadi mkubwa hasa hatua za mwisho za rekodi ya albamu hizo inayomaliziwa jijini Mwanza na baadaye Nairobi,” alisema Msama.
Msama alisema Mwaitege anatarajia kuzindua albamu tatu ambazo zitashika anga la muziki huo hapa nchini kwa sababu ya ubora. Msama alisema sambamba na muimbaji huyo, mikoa mbalimbali imeonesha nia ya kutaka uzinduzi wa albamu hizo.
Aidha Msama alitoa wito kwa mashabiki wa muziki wa Injili Tanzania kujiandaa kupata neno la Mungu kupitia muimbaji huyo. Bonny Mwaitege anatamba na nyimbo mbalimbali kama Mama ni Mama, Mke mwema, Wakusamehe, fungua moyo wako na njoo uombewe na Yesu yupo.(VICTOR)
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment