MKUTANO MKUU WA BARAZA KUU LA SKAUTI TANZANIA 2015 JIJINI DAR ES SALAAM

download (1)
Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la Chama cha Skauti Tanzania unatarajiwa kufanyika jijini D’salaam kuanzia tarehe 13 Agosti hadi 15 Agosti 2015 katika ukumbi wa Karimjee. Mkutano wa Baraza Kuu hufanyika kila baada ya miaka 2 na mara ya mwisho ulifanyika mwaka 2013 jijini D’salaam. Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu utatanguliwa na Semina Elekezi kwa wajumbe wote wa Baraza Kuu, ambao itaanza tarehe 13 na 14 Agosti 2015 na Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu Taifa utafanyika tarehe 15 Agosti 2015.
Wajumbe wote wa Baraza wanatakiwa kuripoti jijini D’salaam tarehe 12 Agosti 2015 jioni. Wajumbe wa Baraza Kuu ni pamoja na Makamishna wote wa Skauti wa Mikoa na Wilaya za Tanzania, Wakufunzi, Viongozi wa Juu wa Chama, pamoja na wageni wengine waalikwa. Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu unatarajia ufunguliwe na Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dk. Jakaya Mrisho Kikwete.
Viongozi wengine wa juu wa Chama ni pamoja na Wadhamini ambao ni Rais Mstaafu wa awamu ya pili Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi, Waziri Mkuu Mstaafu Salim Ahmed Salim na Baba Askofu Timanywa. Rais wa Baraza la Chama cha Skauti Tanzania ni Waziri wa Elimu Mheshimiwa Dk. Shukuru Kawambwa na Makamu wake ni Kaimu Mufti wa Tanzania Alhaji Zuberi, Muadhama Kadinali Polycap Pengo na Profesa Philemoni Sarungi.
Viongozi wengine wa Juu wa Chama ni pamoja na Skauti Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Mwantumu Mahiza, ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mheshimiwa Abdulkarim Shah ambaye pia ni Mlezi: RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Patron: THE PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA P.O. BOX. 945 DAR ES SALAAM, TEL: +255222153342 FAX: + 255 222 150382 EMAIL: tscouts2002@gmail.com TANZANIA SCOUTS ASSOCIATION CHAMA CHA SKAUTI TANZANIA Mbunge wa Mafia na Mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji ya Taifa Mheshimiwa Balozi Mstaafu Nicholas Kuhanga. Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu pamoja na mambo mengine utajadili na kupitisha Katiba ya Chama cha Skauti Tanzania, pamoja na kuchagua wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Taifa.
Fomu za wagombea nafasi hizo tayari zinapatikana Makao Makuu ya Skauti Tanzania yaliyopo upanga, barabara ya Malik, pia katika blog na Tovuti ya Chama ambayo ni www.tanzaniascout.org Mwisho wa kurudisha fomu hizo ni tarehe 7 agosti 2015 saa 9.00 alasiri.
Imetolewa na RASHID K. MCHATTA KNY: KAMISHNA MKUU CHAMA CHA SKAUTI TANZANIA 31/07/2015
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment