PICHA ZAIDI ZA TUKIO LA MKUTANO MKUBWA WA KUMTAMBULISHA MGOMBEA WA UKAWA NDUGU EDWARD LOWASSA MWANZA


Mgombea Urais kupitia UKAWA ndugu Edward Lowassa akiwa na Mgombea mwenza ndugu Juma Duni Hajii katika wa mkutano wa kumtambulisha jijini Mwanza
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akipunga mkono kwa Umati wa wakazi wa Jiji la Mwanza waliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Furahisha, Jijini humo, leo Agosti 16, 2015.


Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Freeman Mbowe akihutubia mamia ya wakazi wa Mwanza wakati wa kumtambulisha Mgombea wa UKAWA jijini Mwanza


Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akihutubia Umati wa Wakazi wa Jiji la Mwanza uliofurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Furahisha, wakati wa Mkutano wa hadhara wa kutafuta wadhamini wa Tume ya Uchaguzi (NEC) kwa wagombea hao na kutambulishwa kwa wananchi, Agosti 16, 2015.


Umati wa Wakazi wa Jiji la Mwanza ukiwa umefurika kwa wingi katika Barabara kuu ya kutoka Uwanja wa Ndege kuelekea katikati ya mji, wakati wa mapokezi wa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa,ambaye yupo kwenye ziara ya kutafuta wadhamini wa Tume ya Uchaguzi (NEC) na kutambulishwa kwa wananchi, leo Agosti 16, 2015.

Umati wa Wakazi wa Jiji la Mwanza ukiwa umefurika kwa wingi kwenye Uwanja wa Furahisha, kulikofanyika Mkutano wa hadhara wa kutafuta wadhamini wa Tume ya Uchaguzi (NEC) na kutambulishwa kwa wananchi, Agosti 16, 2015.

Sunday, August 16, 2015

MAELFU YA WAKAZI WA MWANZA WAMLAKI MH EDWARD LOWASSA

Mgombea urais wa UKAWA Mh. Edward Lowassa ameendelea na ziara yake ya kutafuta wadhani ambapo alianzia jijini Mbeya tarehe 14/8/2015 katika viwanja vya Rwanda nzovwe maarufu kama uwanja wa Dr Slaa na kufuatiwa Jijini Arusha tarehe 15/8/2015 katika viwanja vya Tindigani na kumaliziwa Jijini Mwanza tarehe 16/8/2015 katika viwanja vya Furahisha. Katika mikutano yote hiyo kumekuwa na mwamko mkubwa sana wa wananchi waliojitokeza kumpokea mgombea urais wa UKAWA. Alipotua katika kiwanja cha ndege Mwanza alikutana na umati mkubwa wa watu waliomsindikiza mpaka sehemu ya tukio.
Mbali na kuwa na umati mkubwa wa wafuasi katika mikutano hiyo viongozi wa vyama vinavyounda umoja huo wameendelea kusistiza kuwa Watanzania wajitokeza kwa wingi wao siku ya kupiga kura na walinde kura zao na huku wakitoa matamko mbalimbali juu ya vyombo vya Ulinzi na Usalama kusimamia haki na kulinda usalama wa Watanzania sio kutumika na baadhi ya viongozi kwa maslahi yao binafsi na kuwa hali hiyo ikipuuzwa italeta machafuko katika Taifa.













Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment