Vijana wa Kitanzania waja na king’amuzi cha mtandaoni!

  • Written @nkupamah blog
tango
Vijana watatu wakitanzania ambao kwa ubunifu mkubwa wameweza kuja na wazo ambalo linatekelezeka katika ulimwengu wa teknolojia ya habari na mawasiliano.
Inawezekana ukaanza kutafuta na kuwaza kwamba inawezekanaje tango kuwa televisheni? Hilo ni jina waliloweza kukipa king’amuzi chao kinachoitwa TangoTv.

Vijana hawa wanakuja na teknolojia ya kisasa kabisa ya kukuwezesha wewe kuweza kuangalia filamu zote za hapa Bongo na Afrika kwa ujumla, kupitia kingamuzi chao hicho ambacho kinakupa huduma hiyo kwa kutumia mtandao wa intaneti uliounganishwa moja kwa moja na king’amuzi chao, wala hauhitaji antena.
Vile vile inamaanisha kila sehemu hapa Tanzania ambayo unaweza kupata intaneti ya simu kwa kuanzia 3G, huna shaka kabisa na king’amuzi hiki maeneo kama hayo utapata huduma vizuri.
Vijana hawa ambao wako watatu ambao wameingia kwenye vijana fursa ya kuwa wabunifu bora 30 Afrika katika teknolojia,(Demo Africa Top 30) na wanaipeperusha bendera ya Tanzania. Utofauti wa teknolojia yao ni kwamba wao wameweza kukusanya filamu za kiafrika na kuhakikisha unazipata kupitia king’amuzi chao ambacho kinatumia mtandao wa 4G. 3G, Wifi na pale unapounganisha intaneti ya kawaida mahali popote na wakati wowote.
Ukweli ni kwamba si watu wengi wana uwezo wa kuangalia filamu za bongo au kuzipata kwa urahisi ila kwa teknolojia hii inamaanisha unaweza kuangalia kupitia king’amuzi chao ambacho kimeunganishwa na mtandao wa intaneti huku kikikupa nafasi ya kufuatilia filamu kwenye Youtube. Unaweza kulipia kwa kila filamu unayotaka au kwa mwezi n.k
Teknolojia hii inafanya kazi kwenye televisheni za kawaida ambazo watanzania wengi wanamiliki, cha zaidi ni kwamba unaweza kutumia Tango kwenye kompyuta yako, simu yako n.k
Kuanza mradi huu wamewezeshwa na tume ya sayansi na teknolojia chini ya serikali ya Tanzania ili waweze kuonyesha bidhaa yao ya kwanza na kuweza kuiwezesha kufika sokoni. Kwa sasa unaweza kuweka oda yako kwenye mtandao wao wa www.tangotv.co.tz na hii inaashiria kitu kizuri katika mafanikio yao na teknolojia kwa ujumla wake hapa Tanzania.Kwa upande mwingine ni kwamba wanafanya kitu kipya ambacho ving’amuzi vingine haviwezi kufanya isipokuwa kimoja tu ambacho si cha hapa Tanzania, hiyo kuwapa fursa ya wao kuwa na kivutio kikubwa cha filamu cha Tanzania na zile za kuelimisha ambazo pia ni za kitanzania kwa ajili ya watoto.Je swali ni kwamba wasanii wa filamu za hapa bongo wanalijua hilo? Je wako tayari kunufaika na teknolojia hii ambayo vijana wameweza kuiwaza? Hii inamaanisha kwamba msanii anaweza kutengeneza kazi yake na kuiweka kwenye mtandao wao na kunufaika katika mauzo ya filamu zetu za hapa Bongo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment