SOKA:Henry na Carragher wamshangaa Van Gaal


Nkupamah media
thierry-henry-jamie-carragher-di
Na Rabi Hume, Modewjiblog
Mchezaji wa zamani wa Arsenal, Thierry Henry na mwenzake wa Liverpool, Jamie Carragher ambao kwa sasa ni wachambuzi wa soka katika kituo cha michezo, Sky Sports wamemshangaa kocha wa Manchester United, Louis Van Gaal kwa jinsi anavyomtumia mchezaji wake, Antony Martial.
Wakiwa katika kipindi cha michezo katika kituo hicho wakati wakimzungumzia Martial kwenye mchezo wa
wikiendi iliyopita ambapo Manchester United ilipoteza mchezo huo mbele ya Norwich kwa kipigo cha goli 2 kwa 1 ambapo Henry alionekana kuuliza swali ambalo lilikuwa kama linamlenga kocha Van Gaal kwa kusema “Unafanya nini hapa? Kiukweli sijui anafanya nini pale”.
“Alitakiwa kuwa pale (eneo la penati), akiwa karibu na kipa, anafunga na kushangilia. Ndiyo sawa? Ni kwasababu wana uwezo mdogo sana? Naona hilo,
“Wanahitaji mchezaji ambaye anafunga magoli, wanahitaji mchezaji amabye anaweza kukimbia haraka amekuja na na vitu hivyo, ingawa anatafuta mwenyewe mpira na hagusi kutoka kwa wenzake,
“Nahisi nikiwa na mchezaji kama yeye, atakuwa namba 9 yangu na wengine wote watakuwa nyuma yake,” alisema Henry.
Kwa upande wa Carragher alisema “Hayo ni mapendekezo ya Van Gaal, yeye kucheza pembeni [Martial]. Tusifanye kuwa tumesahau kuwa yule ni mshambuliaji wa kati ambaye ana uwezo wa kuchukua mpira na kukimbia nao akiingia ndani ya eneo la penati”
“Unaangalia mara ngapi anagusa mipira? Hagusi mpira kabisa ndani ya eneo la penati na anapiga mpira mrefu mmoja tu, kwahiyo hana madhara akiwa pembeni na kusababisha mashambulizi langoni kwake,
“Na haya yote yanakuja kwa maelekezo kutoka kwa meneja, na ndiyo maana Manchester United haionekani kuwa ikifunga magoli kwenye michezo yake”
Antony Martial aliwasili Manchester United msimu huu akitokea Monaco ya Ufaransa kwa kitita cha Pauni Milioni 36.7 ambaye alifanikiwa kufunga magoli matano katika michezo yake tisa ya kwanza lakini kwa sasa hali imekuwa ni tofauti kwa kufunga goli mbili katika michezo yake 11 iliyopita.(P.T)
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment