Hali tete Bungeni Dodoma.............Wabunge wa Upinzani Watoka Bungeni tena.......Ni Baada ya Naibu Spika Tulia Ackson Kuwanyima Muongozo ili Waongee

Nkupamah media

Hali ya sintofahamu imeendelea ndani ya bunge baada ya wabunge wote wa Upinzani kutoka ndani ya bunge mara baada ya Wabunge kuanza kuchangia hotuba ya Rais.

Baada ya  kipindi cha Maswali na Majibu, yalifuata matangazo  na   baada ya Matangazo, wabunge wakaanza kuchangia hotuba ya Rais Magufuli .

Wakati hayo yakiendelea, wabunge kadhaa wa UKAWA akiwemo mbunge wa Ubungo(chadema), Saed Kubenea walikuwa wakiomba muongo wa Naibu Spika ili waongee lakini hawakupewa nafasi.

Naibu Spika alikataa miongozo hiyo na kulitaka Bunge lijikite katika kujadili Hotuba ya Rais. Hali hiyo iliwakera wabunge wa upinzani  kwa madai kuwa wamezibwa midomo na hivyo wakaamua kutoka nje yaukumbi wa bunge

==>Wabunge wa CCM wanaendelea  kujadili Hotuba ya Rais.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment