Aliyasema hayo jana wakati wa kongamano la wazi juu ya changamoto za kisheria zilizojitokeza baada ya kufutwa kwa uchaguzi mkuu wa Zanzibar uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana, lililoandaliwa na Chama Cha Wanasheria Tanganyika (TLS), jijini Dar es Salaam jana.
Alisema endapo kamati hiyo itabaini kuwa hakukuwa na uhalali wa kufutwa kwa uchaguzi huo, waliohusika kufutwa watatakiwa kufikishwa katika mikono ya sheria.
“Zaidi ya mikutano 172 ilifanyika nje ya muda uliopangwa, kwa mujibu wa utafiti tuliofanya katika mikoa mitano ya Dar es Salaam, Tabora, Arusha, Mbeya na Tanga, wanasisasa wengi hawakufuata sheria ya muda,” alisema Sungusia.
Alisema viashiria vya rushwa pia vilitawala katika uchaguzi huo, ambapo zaidi ya mikutano 139 kulikuwa na viashiria vya rushwa na changamoto nyingine waliyobaini ni ucheleweshwaji wa kutangaza matokeo katika baadhi ya vituo vya kupigia kura.
Alisema bila ya kuwapo kwa vitu hivyo hali mbaya ya kisiasa visiwani humo inaweza kujirudia kila uchaguzi utakapofanyika.
Alisema viongozi wa bara kujiweka pembeni katika mgogoro huo unaendelea visiwani humo kunaweza kuudhofisha muungano.
-
Blogger Comment
-
Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)









0 comments :
Post a Comment