Mwongozo mpya wa unywaji pombe kutolewa

Pombe
Maafisa wa afya nchini Uingereza wanatarajiwa kutoa mwongozo mpya kuhusu unywaji pombe, ambapo watapendekeza watu kutokunywa pombe angalau siku mbili kwa wiki.
Mwongozo huo utatolewa baada ya
kutathminiwa upya kwa mwongozo wa awali uliotolewa miaka 20 iliyopita.
Ripoti zinasema afisa mkuu wa matibabu Uingereza Sally Davies atapendekeza watu wawe wakijizuia kunywa pombe angalau siku mbili kwa wiki.
Kiwango salama cha wanaume kunywa kwa siku pia kitapunguzwa na kufikia kilichopendekezewa wanawake.
Kwa sasa, wanawake hushauriwa kutokunywa zaidi ya vipimo 2-3 (sawa na gilasi ya mililita 175 ya mvinyo) kwa siku na wanaume vipimo 3-4.
Kipimo kimoja cha kileo ni sawa na nusu painti ya pombe isiyo kali sana au lager ya 4.5%, au mililita 25 za pombe kali.
Gilasi moja ya mililita 175 ya divai ya ukali wa 12% ina vipimo 2.1 na painti ya bia kali (ABV 5.2%) ina vipimo vitatu.
Kiwango kilichopendekezwa
Pombekwa wanawake kilikuwa chini
Kwa mujibu wa ripoti katika vyombo vya habari Uingereza, mwongozo huo mpya utasisitiza kwamba hakuna unywaji pombe “salama” na kwamba hata kunywa viwango vidogo vya pombe kunaweza kusababisha saratani.
Mwongozo nchini Scotland tayari hushauri watu kujizuia kunywa pombe angalau siku mbili kwa wiki.
Mwongozo huo wa unywaji pombe ulianzishwa 2013 baada ya Idara ya Afya Uingereza kusema ilikuwa imepokea “malalamiko” kutoka kwa wataalamu wakipendekeza uchunguzi wa kina kuhusu pombe na afya.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment