Mchezaji
Bora wa Afrika wa wachezaji wanaocheza ligi za ndani na nahodha wa timu
ya taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta ametuma picha katika ukurasa wake
wa Twitter akiwasili mji mkuu wa Ubelgiji, Brussels kwa ajili ya
kukamilisha dili lake la kujiunga na klabu ya Genk.
Safari
ya Samatta nchini humo imekuja baada ya klabu yake ya TP Mazembe
kuridhia mchezaji huyo kujiunga na Genk ambapo awali ilionekana kutokuwa
tayari kumuachia nyota
huyo wa wachezaji wa ligi za ndani Afrika ambaye
mkataba wake na TP Mazembe ulikuwa ukimalizika mwezi Aprili.
0 comments :
Post a Comment