Wadau wakutana kujadili njia mahususi za kuboresha mazingira na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kwenye majiji



 
Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu Rais, Ngosi Mwihava akifungua
mkutano huo wa wadau ambao umewashirikisha pia watendaji wa serikali na
mashirika yasiyo ya serikali kutoka katika wizara na idara mbalimbali,  kwa lengo la kujadili kwa
pamoja namna ya
kushirikiana na kupata njia ya pamoja ya kuboresha mazingira na kukabiliana na
athari za mabadiliko ya tabianchi zikiwemo mafuriko, magonjwa na uharibifu wa
miundombinu.

Wadau wakifuatilia Mkutano huo
 Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu Rais, Ngosi Mwihava (katikati)
akiwa na viongozi wa Forumcc wakati wa mkutano huo, kuanzia kushoto ni Mkurugenzi
Msaidizi anayeshughulikia Mabadiliko ya Tabianchi katika Ofisi ya Makamu wa
Rais, Richard Muyungi, Mkurugenzi wa Mazingira katika Ofisi ya Makamu wa Rais,
Julius Ningu wakati kuanzia kulia ni Afisa Miradi Forumcc, Fazal Issa na Mwenyekiti
wa bodi ya forumcc, Yusta Kibona
 Mkurugenzi wa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Dr.
Julius Ningu akifafanua jambo wakati wamkutano huo
Meneja Miradi Forumcc, Rebecca Muna akielezea jambo wakati wa mkutano huo
 Picha ya pamoja
 Profesa Robert Kiunsi kutoka Chuo cha Ardhi akiwasilishwa
mada kuhusu atharai za mabadiliko ya tabianchi na namna ya kubabiliana na
athari hizo
 Amy Faust Kutoka Benk ya Dunia akiwasilisha mada ya mifano
ya miradi ya kuboresha mazingira katika majiji ilivyofanikiwa katika nchi
nyingine huko Ulaya, mifano ambayo inaweza kutumiwa pia hapa nchini
 Francis Gowele, Afisa Mazingira Manispaa ya Ilala akitoa
report ya mazingira katika manispaa hiyo
 Mwezeshaji wa mkutano huo Abdallah Henku akielezea jambo
wakati wa mkutano huo
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment