Ripoti za raia wa Somalia zinasema kwamba wanajeshi wa Umoja wa Afrika wanaoshirikisha wanajeshi wa Uganda wameondoka katika kambi moja katika mji wa
bandari ya zamani wa Marka,kusini mwa mkoa wa Shebelle ya chini.
Kambi hiyo ipo kilomita 109 kusini magharibi mwa mji mkuu wa Mogadishu.
Ripoti nyengine zinasema kuwa wapiganaji wa alshabaab walionekana wakiinua bendera yao katika mji huo.
Hatua hii inajiri wakati ambapo wanajeshi wa Kenya wamejiondoa katika kambi kadhaa katika eneo jingine la kusini mwa taifa hilo kufuatia shambulio katika kambi ya el-Ade mwezi uliopita.
IMECHOTWA KWENYE MTANDAO WA BBC
0 comments :
Post a Comment