Usharobaro Wamtokea Puani Stan Bakora

Nkupamah media:

Usharobaro umemtokea puani komediani wa Bongo, Stanley Yusuph ‘Stan Bakora’ baada ya kudondoka na kuumia mguu wa kulia wakati akifanya mazoezi ya kutumia Cyboard (Saibodi).

Ishu nzima ilitokea wiki iliyopita katika moja ya duka la nguo lililopo Kinondoni, Dar baada ya kupiga mwereka wa kufa mtu na kujikuta akianguka kama mkungu wa ndizi kutoka juu ya mgomba kisha kuumia mguu.

“Hicho kidude, kwangu ni kigeni ndiyo nilikuwa nakijaribisha nione inakuwaje ndipo nilipoanguka kama mara mbili hivi na kuumia mguu wa kulia, kiukweli kimenitoa ushamba,” alisema Stan Bakola.

Chanzo:GPL
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment