Mchezaji
 Bora mara tano wa tuzo ya Ballon d’Or, Lionel Messi amefunguka na 
kuweka wazi kuwa anazipenda ligi za Uingereza na Italia.
Messi
 alisema hayo wakati akizungumza na kituo cha tv cha Misri, MBC na 
kueleza kuwa licha ya kuzipenda ligi hizo bado anataka kusalia Barcelona
 kwa maisha yake ya soka kabla ya kuhamia katika timu yake ya utotoni, 
Newell’s Old Boys.
“Ninapenda
 mpira wa Uingereza na Italia” alisema na kuongeza “Huwa natazama 
michezo mikubwa lakini nilishasema ninataka kuendelea kuchezea Barcelona
 kwa miaka mingi na hadi nitakapostafu”
Awali
 kabla ya Messi kuzungumzia jambo hilo amekuwa akihusishwa kujiunga 
Manchester City na dili hilo linaonekana kuwa rahisi kukamilika kutokana
 na kocha wake wa zamani, Pep Guardiola kujiunga na Manchester City 
baada ya msimu huu kumalizika.


0 comments :
Post a Comment