Mchezaji
Bora mara tano wa tuzo ya Ballon d’Or, Lionel Messi amefunguka na
kuweka wazi kuwa anazipenda ligi za Uingereza na Italia.
Messi
alisema hayo wakati akizungumza na kituo cha tv cha Misri, MBC na
kueleza kuwa licha ya kuzipenda ligi hizo bado anataka kusalia Barcelona
kwa maisha yake ya soka kabla ya kuhamia katika timu yake ya utotoni,
Newell’s Old Boys.
“Ninapenda
mpira wa Uingereza na Italia” alisema na kuongeza “Huwa natazama
michezo mikubwa lakini nilishasema ninataka kuendelea kuchezea Barcelona
kwa miaka mingi na hadi nitakapostafu”
Awali
kabla ya Messi kuzungumzia jambo hilo amekuwa akihusishwa kujiunga
Manchester City na dili hilo linaonekana kuwa rahisi kukamilika kutokana
na kocha wake wa zamani, Pep Guardiola kujiunga na Manchester City
baada ya msimu huu kumalizika.


0 comments :
Post a Comment