Licha
ya kuibuka na ushindi wa goli moja kwa bila dhidi ya timu mpya ya Rafa
Benitez, Newscastle United, Leicester City imevunja rekodi aliyokuwanayo
kocha Benitez tangu Agosti, 2001.
Benitez
alikuwa na rekodi ya kutokupoteza mchezo wa kwanza katika timu
alizofundisha ambazo ni Valencia, Liverpool, Inter Milan, Chelsea,
Napoli na Real Madrid.
Goli
lililomaliza historia hiyo ya miaka 15 lilifungwa na Shinji Okazaki,
goli limeloisaidia Leicester kufikisha alama 63 ikiwa katika nafasi ya
kwanza.


0 comments :
Post a Comment