McCLAREN ATIMULIWA, BENITEZ KURITHI?


Steve McClaren amefukuzwa kazi kama Meneja wa Newcastle Unite.McClaren, mwenye Miaka 54, ametolewa kwenye wadhifa huo baada ya Miezi 9 huku Newcastle ikiwa Nafasi ya 19 kwenye Ligi Kuu England ikiwa ni nafasi 1 tu juu ya Timu ya mkiani Aston Villa.
Tangu McClaren atwae wadhifa huo mwanzoni mwa Msimu huu Newcastle imeshinda 7 tu kati ya 30.
Mechi ya mwisho kwa McClaren ilikuwa Jumamosi iliyopita Newcastle wakiwa kwao St James Park na kupigwa 3-1 na Bournemouth ikiwa ni kipigo chao cha 5 katika Mechi 6 zilizopita.
Habari za ndani ya Newcastle zinamtaja Rafael Benitez, Meneja wa zamani wa Chelsea, Liverpool na Real Madrid, kumrithi McClaren.
Inaaminika Muhispania huyo huenda akateuliwa haraka na kutwaa wadhifa kabla Newcastle haijasafiri kwenda huko King Power Stadium Jumatatu Usiku kucheza na Leicester City.(VICTOR)
ENGLAND – Ratiba Mechi za Wikiendi
**Saa za Bongo
Ijumaa Machi 11
EMIRATES FA CUP – Raundi ya 6 [Robo Fainali]
2255 Reading v Crystal Palace
Jumamosi Machi 12
LIGI KUU ENGLAND
1545 Norwich v Man City
1800 Bournemouth v Swansea
1800 Stoke v Southampton
EMIRATES FA CUP - Raundi ya 6 [Robo Fainali]
2030 Everton v Chelsea
Jumapili Machi 13
LIGI KUU ENGLAND
1900 Aston Villa v Tottenham
EMIRATES FA CUP - Raundi ya 6 [Robo Fainali]
1630 Arsenal v Watford
1900 Man United v West Ham
Jumatatu Machi 14
LIGI KUU ENGLAND
2300 Leicester City v Newcastle
Share on Google Plus

About Mng'atuzi blog

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment