Nkupamah media:
Alisema sambamba na fao hilo, katika mkutano mkuu wa saba ya mwaka huu, mfuko huo unatarajia kuzindua utaratibu wa maisha popote na LAPF ikiwa ni mikakati ya mfuko huo kupanua huduma.
Akizungumzia hali ya mfuko huo, mkuu wa kitengo cha tathmini ya mfuko , Abubakar Ndwata alisema hadi sasa mfuko una wanachama 156,000 na ukiwa na thamani ya Sh1.087.Trilioni
Mkurugenzi mkuu wa mfuko wa
pensheni wa LAPF Eliudi Sanga akizungumza katika mkutano huo ambapo
alisema kuwa Mifuko ya hifadhi ya jamii imekua chachu ya maendeleo ya
taifa kutokana na uwekezaji unaofanywa na mifuko hiyo pamoja na mikopo
mbalimbali inayotolewa kwa wanachama kujikwamua kimaisha.
………………………………………………………………………………………………………………….
Mahmoud Ahmad Arusha
Arusha,Mfuko wa Pensheni wa LAPF ,
umetoa mkopo wa sh 1.2 bilioni kwa watumishi 800 ambao ni wanachama
wa mfuko huo katika kipindi cha mwaka 2015/16 ili wajiendeleze kielimu.
Mkuu wa kitengo cha masoko na
mawasiliano wa mfuko huo, James Mlowe alitoa taarifa hiyo jana, wakati
akizungumza na waandishi juu ya mkutano mkuu wa mwaka wa mfuko huo
ambao unatarajiwa kufanyika jiji hapa kuanzia Machi 10 mwaka huu.
Mlowe alisema, mfuko huo ulizindua fao hilo la elimu mwaka
jana ambalo sasa limekuwa na manufaa makubwa kwa watumishi ambao
wanataka kujiendeleza.Alisema sambamba na fao hilo, katika mkutano mkuu wa saba ya mwaka huu, mfuko huo unatarajia kuzindua utaratibu wa maisha popote na LAPF ikiwa ni mikakati ya mfuko huo kupanua huduma.
Akizungumzia hali ya mfuko huo, mkuu wa kitengo cha tathmini ya mfuko , Abubakar Ndwata alisema hadi sasa mfuko una wanachama 156,000 na ukiwa na thamani ya Sh1.087.Trilioni
Alisema makusanyo kwa mwaka uliopita ni sh 203 bilioni ambapo malipo kwa mwaka jana ilikuwa ni Sh 88 bilioni.
Akizungumzia mkutano alisema
mgeni rasmi anatarajiwa kuwa waziri wa nchi ofisi ya Rais, Tawala za
mikoa na serikali za mitaa, George Simbachawene.
Alisema katika mkutano huo, mada
mbali mbali zitatolewa ikiwepo taarifa ya mfuko, taarifa ya fedha,
mipango ya uwekezaji na ugonjwa wa Tezi dume.


0 comments :
Post a Comment