Yanga, Azam fc zashinda ugenini Kimataifa katika michezo yao ya leo Machi 12


Timu za Tanzania zinazoshiriki michuano ya Kimtaifa kwa ngazi ya vilabu ikiwemo Azam na Yanga katika michezo yao leo Macho 12.2016 zimeweza kuchomoka na ushindi ugenini  hali ambayo zinajiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele zaidi kwenye michuano hiyo.
Yanga wao wamweza kuchomoka na ushindi wa bao 2-1 dhidi ya wapinzani wao, Warwanda, Klabu ya APRA ambayo ni ya Jeshi. Kwa upande wa Azam wao wamepata ushindi huo usiku huu baada ya kuifunga bao 3-0 dhidi ya wapinzani wao Bidvest Wits ya Afrika Kusini kwenye mchezo wa kombe la shirikisho ikiwa ni saa chache baada ya Yanga kupata ushindi  huo wa magoli 2-1 dhidi ya APR Kigali, Rwanda.
Azam walipata bao la kwanza lilifungwa na Salum Abubakar ‘Sure Boy’ dakika ya 50 baada ya kuachia shuti kali nje ya 18 kufuatia kona iliyopigwa na Ramadhani Singano ‘Messi’ kuokolewa vibaya na mabeki wa Wits kisha mpira kumkuta Sure Boy.
Dakika ya 57 baadaye, beki wa pembeni wa Azam FC Shomari Kapombe aliipatia Azam bao la pili baada ya mabeki wa Wits kufanya uzembe kuokoa mpira kisha Kapombe akaserereka na kupiga mpira uliotinga moja kwa moja kwenye kamba za Wits. John Bocco ‘Adebayor’ alihitimisha kipigo hicho kwa kufunga bao la ushindi dakika ya 60 na kuiweka Azam kwenye mazingira ya kusonga mbele mbele kwenye michuano hiyo.
YANGAZKikosi cha Yanga. Yanga wamepata ushindi wa bao 2-1 dhidi ya APRA, nchini Kigali-Rwanda.
AZAMBaadhi ya wachezaji wa Azam wakipongezana baada ya John Bocco kupachika bao katika mchezo uliocheza usiku huu Machi 12.2016, nchini Afrika Kusini.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment