Mwafrika wa Kwanza Kushinda Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Kulipwa Ulaya Ametangazwa, Amewahi Kuifunga Tanzania


Usiku wa April 24 imetangazwa good news  kwa soka la Afrika, huu sio ushindi wa taifa la mchezaji husika ila  ni fahari ya Afrika nzima, winga mshambuliaji wa kimataifa wa Algeria anayeichezea klabu ya Leicester City ya Uingereza Riyad Mahrez ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya PFA 2015/2016 (Professional Footballers Association).

Riyad Mahrez ametangazwa kushinda tuzo hiyo mbele ya wachezaji kama Mesut Ozil wa Arsenal, Jamie Vardy wa Leicester City, Harry Kane wa Spurs, N’golo Kante wa Leicester City, Dimitri Payet wa West Ham United, PFA ni tuzo za wachezaji bora wa kulipwa.

Kama utakuwa unakumbuka vizuri Riyad Mahrez ndio alikuwa mchezaji wa Algeria aliyefunga goli la nne dakika ya 43 katika ushindi wa goli 7-0 dhidi ya Taifa Stars November 17 2015 na kuIondoa Tanzania katika mbio za kuwania kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2018.
Share on Google Plus

About Mng'atuzi blog

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment