Soma tamko la OJADACT juu ya waandishi kuzuiwa kuingia Bungeni

Ndugu waandishi wa Habari, wanaharakati na watanzania wote.
Chama cha Waandishi wa Habari wa Kupiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uhalifu Tanzania (OJADACT). Tunalaani vikali kuzuiwa kwa Waandishi kuingia Bungeni kwa lengo la kufanya coverage ya vikao vya Bunge la kujadili mpango wa maendeleo ya miaka mitano na bajeti ya serikali.
OJADACT, hatukubaliani na utaratibu wa sasa wa kutumia idara ya habari na maelezo ya Bunge, kuwa ndio wenye jukumu la kukusanya taarifa na kuzigawa kwa waandishi.
Ni ukweli usiopingika kuwa, maamuzi hayo yana athari zifuatazo.
Kuminya uhuru wa haki ya kupata taarifa kwa wananchi km ilivyoainishwa kwenye katiba ya Jamhuri ya Muungano.wa.Tanzania ibara ya 18.
Kuminya uhuru wa vyombo vya habari, ambao umekuwa ukikosa haki ya msingi iliyokosekana kwenye Katiba.
MSIMAMO WETU. 1: Kwa kuwa Bunge halioni umuhimu wa waandishi Bingeni basi tunaviomba vyombo vyote vya habari vya binafsi kuwatoa waandishi wao bungeni.
Tunaviomba vyombo vyote vya habari vya binafsi kususia kuandika habari za bunge hadi hapo litakapotengua utaratibu huo.
Waziri mwenye dhamana ya habari afute kauli yake ya kejeli kuwa wanaopinga utaratibu huo eti waende Mahakamani.
Ahsanteni sana wanahabari kwa kuotokia wito wetu.
Edwin Soko Mwenyekiti (Pichani).
Share on Google Plus

About Mng'atuzi blog

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment