KINSHASA,
CONGO: Mwili wa mwimbaji nguli wa muziki wa dansi nchini DR Congo, Papa
Wemba, unatarajiwa kuzikwa leo katika kijiji chaa Molokai kama kawaida
kufuatia kuomba hivyo kwa ndugu na jamaa wa wanamuziki huyo hapo awali.
Tayari
upande wa Serikali na kamati ya mazishi ya msanii huyo iliweza kutoa
siku tatu za maombelezo na kuaga kwa ndugu na jamaa ambapo pia Serikali
ya Nchi hiyo kupitia kwa Rais wake Joseph Kabila aliweza kumtunukia tuzo
ya heshima ya juu katika nchi pamoja na kutoa siku tatu za maombelezo
ambayo ilianza juzi na leo hii kutakuwa na maziko rasmi.
Papa
Wemba alifariki hivi karibuni jijini Abidjan nchini Ivory Coast ambapo
awali alipoteza fahamu akiwa jukwaani alipokuwa akitumbuiza baada ya
kuanguka na kukimbizwa hospitali.
0 comments :
Post a Comment