Utafiti wadai mtu mmoja kati ya wanne ni kichaa, Wizara yaeleza sababu

Mix


Gazeti la Jambo leo limeripoti kuwa Waziri wa afya, maendeleo ya jamii, jinsia, watoto na wazee, Ummy Mwalimu amesema utafiti unaonesha kuwa kwa kila watu wanne duniani , mmoja ana matatizo ya afya ya akili.
Kwa mujibu wa Waziri Ummy wananchi wanapaswa kuwa makini kuchunguza afya zao za akili  kwa sababu utafiti wa shirika la afya duniani ‘WHO’ zinaashiria kuwa jamii kwa sasa inakumbwa na maradhi mengi ya namna hiyo, Waziri Ummy alibainisha 
>>>’Miongoni mwa watu wanaopata matatatizo ya kiakili ni wachache  tu ambao wanaweza kufikia na kupata huduma ya afya ya akili, hata hao wanohudhuria vituo vya afya, ni wachache wamekuwa wakipata huduma stahiki’
Alifafanua sababu za kijamii zinazoweza kusababisha mtu kupata magonjwa ya akili ni umaskini uliokithiri, kutengwa na kubaguliwa na jamii. sababu nyingine alizitaja kuwa ni kunyanyaswa kimwili na kingono, kuwa tegemezi, kupoteza mali, kazi, ulevi, kukosa huduma muhimu na unyanyapaa.
Source: Jambo Leo
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment