Rais wa Zanzibar Dr Shein Afanya Uteuzi Wa Wakuu Wa Wilaya Na Mikoa



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dk. Ali Mohamed Shein amefanya uteuzi wa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kama ifuatavyo:
1. UTEUZI WA WAKUU WA MIKOA
Kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu 61(1) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dk. Ali Mohamed Shein amefanya uteuzi wa Wakuu wa Mikoa kama ifuatavyo:
 
i. Mkuu wa Mkoa wa Mjini na Magharibi – Mheshimiwa Ayoub Mohamed Mahmoud
ii. Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini, Unguja – Mheshimiwa Vuai Mwinyi Mohamed
 
Aidha Wakuu wa Mikoa ambao Mikoa yao haikutajwa katika taarifa hii wanaendelea na dhamana zao kama kawaida.
Uteuzi huo umeanza tarehe 23 Mei 2016.
 
2. UTEUZI WA WAKUU WA WILAYA
Kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu 61(2) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dk. Ali Mohamed Shein amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya kama ifuatavyo:
 
i. Mkuu wa Wilaya ya Mjini – Mheshimiwa Marina Joel Thomas.
ii. Mkuu wa Wilaya ya Magharibi “B” – Mheshimiwa Silima Haji Haji
iii. Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini “A”– Mheshimiwa Hassan Ali Kombo
iv. Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini “B” – Mheshimiwa Issa Juma Ali
v. Mkuu wa Wilaya ya Kati – Mheshimiwa Mashavu Sukwa Said
vi. Mkuu wa Wilaya ya Kusini – Mheshimiwa Idrissa Kitwana Mustafa
vii. Mkuu wa Wilaya ya Chakechake – Mheshimiwa Salama Mbarouk Khatib
 
Aidha Wakuu wa Wilaya ambao Wilaya zao hazikutajwa katika taarifa hii wanaendelea na dhamana zao kama kawaida.
 
Uteuzi huo umeanza leo tarehe 23 Mei 2016.
 
Viongozi wote waliotajwa wanatakiwa waripoti Ikulu, Mjini – Unguja, siku ya Jumanne tarehe 24 Mei 2016 saa 8 za mchana tayari kwa kuapishwa.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment