Video ya dakika 7 Ikimuonyesha Waziri Kitwanga akijibu swali huku amelewa Bungeni




Rais  wa Jamhuri  ya  Muungano  wa  Tanzania Dr. John P. Magufuli jana  alitengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Charles Kitwanga  kufuatia kitendo cha waziri huyo kuingia bungeni na kujibu swali linaloihusu wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi akiwa amelewa.

Jana, Kitwanga alijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Devotha Minja lililosomwa kwa niaba yake na Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Suzan Kiwanga na maswali na majibu yake yalikuwa kama ifuatavyo:
 
Suzan: “Miaka 55 Wilaya ya Kilombero polisi hawana nyumba wamepanga na Jimbo la Mlimba wanaishi kwenye nyumba za Tazara. Tuwape miaka mingapi mjenge nyumba na vituo vya polisi?
 
Kitwanga: Kwani wewe una miaka mingapi? Usiulize miaka ya kujenga nyumba za polisi na vituo. Amini tutajenga tu. Halafu wewe ni rafiki yangu lazima nikujibu hivyo.”
 
Suzan: Waziri unajibu kwa mapozi sana (kicheko bungeni). Huku Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe akionekana kucheka zaidi.

==>Hapa chini kuna Video ya dakika 7 ikimuonyesha Waziri huyo  akijibu swali huku amelewa
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment