Kiungo
mkabaji kutoka Kenya, Victor Wanyama anayekipiga katika klabu ya
Southampton ya England anataraji kujiunga Tottenham baada ya kuwepo kwa
taarifa kuwa klabu hiyo inayoongozwa na meneja wake wa zamani
inamuhitaji.
Mitandao
mbalimbali ya michezo barani Ulaya imeripoti kuwa tayari Southampton
wamethibitisha uhamisho huo na kinachosubiriwa ni Wanyama kufanyiwa
vipimo kisha kuhamia Tottenham.
Wanyama
ambaye amesalia na mkataba wa mwaka mmoja na klabu yake ya sasa,
Southampton, uhamisho wake wa kuhamia Tottenham unatajwa kufikia kiasi
cha Pauni Milioni 12.
Kama
Wanyama usajili wake ukikamilika basi kuanzia msimu ujao ataanza tena
kuonekana katika Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya mara ya mwisho kucheza
michuano hiyo mikubwa Ulaya kwa vilabu kipindi akiwa na Celtic kabla ya
kuhamia Southampton.


Blogger Comment
Facebook Comment