Zikiwa
zimesalia siku chache kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa 2016/2017
katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL), beki wa kati wa Manchester United,
Daley Blind amefunguka kuhusu nafasi yake katika kikosi cha kocha
Mourinho.
Blind
alisema ugumu huo unatokana na ujio wa kocha mpya katika klabu hiyo
ambaye ana mfumo wake na ujio wa wachezaji wapya ambapo kwa upande wa
nafasi ambazo anacheza yeye tayari amesajiliwa Eric Bailly na hivi
karibuni Paul Pogba anataraji kuwasili.
Alisema
ili anajiamini kuwa ana kiwango kizuri lakini anahitajii kufanya
mazoezi zaidi ili kufanya vizuri zaidi pindi anapopatiwa nafasi ya
kucheza.
“Ninajiamini
na uwezo wangu na ninatakiwa kuonyesha zaidi na zaidi, nadhani kwa
michezo ya kuajiandaa na msimu mpya mpaka sasa nimefanya kazi kubwa na
nitaendelea kuongeza juhudi,
“Bado
hajasema jambo kuhusu mimi na hata watu wengine, nahitaji kufanya
mazoezi kwa bidii na kupata nafasi katika timu. Nafikiri kila mwalimu
ana mawazo yake, huyu ni kocha mkubwa na mipango yake na kama timu
tunajifunza mengi,” alisema Blind.


Blogger Comment
Facebook Comment