Ndugu JPM, milimoni? Dodoma, mji mzuri wenye mengi mazuri.
Ndoto za Dodoma za Baba wa Taifa, kijana wa Mwitongo Juliasi Nyerere, si ndoto tena bali uhalisia Safari imeanza, na mabegi tayari tumebeba.
Tatizo, uzuri wa Dodoma umeingia shubiri Si kwa kasi hii Kubwa, si kupinga fikra zako sahihi kama Mwenyekiti wa Chama na AmiriJeshi Mkuu Bali ni vipele vilivyogeuka majipu kwenye mahusiano Kumbuka zile semina na mikutano ya nenda lala siku mbili Dodoma urudi Ijumaa ilikuwa ni homa kali kwenye mahusiano.
Ndugu JPM, Mahusiano ndio msingi wa nguvukazi ya taifa. Wafanyakazi wanapokua wametulizwa kwenye mahusiano, huweza kufanya kazi kwa bidii na kasi ya kustaajabisha.
Yaani ukisema hapa kazi tu, wala hawashangai. Nasema kutoka moyoni, maana msema ukweli ni mpenzi wa Mungu. Safari ya Dodoma ni maumivu kwa mahusiano machanga na yale makongwe
Inawezekana kujipanga kwenda baadae kidogo BABA?. Tunaomba nafasi ya kupanga utaratibu wa mahusiano, yaani kujua tunayaweka-wekaje. Sijui kama unajua ndugu JPM, Kwa tamko lako tu kwamba asiyetaka safari ya Dodoma, atafute ajira mbadala, uhusiano, uchumba, ndoa zote ni sawa na talaka tatu, hakuna rejea.
Yaani ni kama vile ng’ombe wa masikini hazai. Unajua mahusiano mengi yalikuwa yanawezeshwa na vile vinanihii, maana misongo ya utumbuaji majipu ni balaa
Wala havikuwa vinachochea yale mengine. Wahusika wa yale mambo wanajulikana .. Tuwatafute hao
Sasa marufuku imetangazwa kwa vilinda mahusiano na ndoa
Kwa wanawake na wanaume, mambo ni ngumu zaidi hasa wale walio safarini kuelekea Idodomya
Mkuu, tembeza huruma yako, mioyo ya watu ipate kupumua maana ingekuwa uhamisho wa mtu mmoja mmoja ni msiba binafsi, huu wa jumla ni kilio nyumba kwa nyumba mtaani
tunakuja Dodoma
yaiya
13667872_10154940206507788_195409789957240951_oPichani ni baadhi ya vijana wakicheza ngoma ya kabila la Wagogo ambao ni wenyeji wa hasili wa Mkoa wa Dodoma
13920708_10154940207577788_7134849715097873342_n
13668821_10154940206917788_7318259275716170072_oMnara wa kumbukumbu wa Nyerere uliopo Dodoma Mjini