Tangawizi
ni kiungo muhimu katika chakula ambacho asili yake ni katika maeneo ya
kitropiki ya kusini mwa bara la Asia, kiungo hichi pia kinadhaniwa kuwa
kina asili ya ukanda wa nchi ya India
Tangawizi
iliweza kufika Afrika kama tokeo la biashara ya nafaka na mazao baina
ya bara la Asia na Afrika enzi za ukoloni, japokuwa zipo taarifa za
kihistoria zinazoeleza kuwa Tangawizi ilikuwepo Afrika ila watu hawakuwa
na ufahamu nayo wala matumizi.
Kiungo
hichi muhimu kina matumizi mbalimbali yanayotegemea kusudio la mtu
mwenyewe kwani Tangawizi hutumika kutengenezea siki au sherry, wengine
hutengeneza vitafunwa kama biskuti /kuki(bites/biscuits,cookies) au
kupikwa kama kiungo katika vyakula vingi. Lakini pia tangawizi inaweza
kutengeneza pipi, mvinyo na vingine vingi.
Wengine hupenda kutumia kiungo hichi katika upishi wa chai na utengenezaji wa sharubati/juisi (juice)
Lakini
pia katika sekta ya afya Tangawizi ina historia ndefu ya matumizi kwa
kupunguza matatizo ya utumbo kama vile kichefuchefu, kupoteza hamu ya
kula, ugonjwa mwendo na maumivu.
Tangawizi
ilianza kutumika mashariki ya mbali, kama vile China na India wakitumia
kwa kutibu maradhi mbali mbali. Katika hili zao la tangawizi kuna
vyanzo vya:
-Magnesium
-Manganese
-Potasium
-Copper
-Vitamini B6
katika mwili wa binaadamu wataalam na wagunduzi wanasema kuwa Tangawizi ni tiba tosha kwa magonjwa mengi
-Husaidia kutibu magonjwa ya ngozi
-Husaidia kupunguza kama si kuondoa kichefuchefu ni nzuri haswa kwa wale wanawake wenye mimba changa ambao husumbuliwa kutapika.
-Husaidia
wale wenye matatizo ya gauti yaani sehemu ya viungo kuuma na kusikia
maumivu makali kupata ahueni, pia husaidia kusambaza damu kwenye mwili
kwa haraka zaidi.
-Husaidia msago wa chakula kwa haraka zaidi kwa kuchanganya na tindikali tumboni.
-Husaidia kwa wale wanaosafiri baharini ikiwa na machafuko kuzuia kutapika,kwa kutumia nusu saa kabla ya kusafiri na boti.
-Husaidia kupigana na kukinga kansaa ya kizazi.
-Tangawizi husaidia kupunguza maumivu mwilini
-Husaidia kutoganda kwa damu mwilini
-Wataalamu wamegundua tangawizi ni dawa tosha ya presha kuliko kitunguu swaumu.
-Husaidia kuponya mafua kwani chai ya tangawizi ni salama


0 comments :
Post a Comment