Baada
ya kufutwa uanachama aliyekuwa mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF)
Profesa Ibrahim Lipumba, Baraza Kuu la Uongozi CUF linatarajiwa kuanza
kazi rasmi Ijumaa ya Septemba 30,2016.
Kabla
ya Lipumba kurejea katika wadhifa wake wa Uenyekiti siku za hivi
karibuni baada ya kujiudhuru mwaka jana, baraza hilo lilikuwa
linakiongoza chama hicho.
Wanachama
wa CUF wa mkoa wa Dar Es Salaam kwa kushirikiana na Wabunge wote wa
CUF, wameandaa mapokezi makubwa siku ya Ijumaa kuanzia saa 2.00 asubuhi
ambapo watawakaribisha Wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi Taifa katika
Ofisi Kuu za CUF Buguruni jijini Dar es Salaam.
Wajumbe hao walikuwepo Zanzibar kwenye Kikao Maalumu ambacho kililenga kutengeneza mustakabali muhimu wa chama hicho.
Mameya
wa CUF, Madiwani, Kamati ya Uongozi ya Chama, Katibu Mkuu, Wakurugenzi,
Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Chama watawasili katika ofisini za
chama hicho na kuanza kazi rasmi.


0 comments :
Post a Comment