WAWAKILISHI WAMKUMBUKA NA KUMLILIA JUMBE..!!!


» » WAWAKILISHI WAMKUMBUKA NA KUMLILIA JUMBE..!!!

WAJUMBE wa Baraza la Wawakilishi wamekaa kimya kwa muda wa dakika moja kumkumbuka aliyekuwa Rais wa awamu ya pili ya Zanzibar, Aboud Jumbe Mwinyi aliyefariki mwezi uliopita ambaye alikuwa muasisi na mwanzilishi wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, ambacho ni chombo cha kutunga sheria.

Spika wa Baraza la Wawakilishi, Zubeir Ali Maulid alisoma wasifu wa Mzee Jumbe na kusema atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika kukuza na kuimarisha demokrasia, ikiwemo kuanza kwa harakati za kutungwa kwa katiba ya kwanza ya Zanzibar ya mwaka 1979 pamoja na kuanzishwa kwa Baraza la Wawakilishi katika mwaka 1980.
“Huo ndiyo mchango mkubwa wa Jumbe katika harakati za demokrasia Zanzibar ambayo ilifanya kuanzishwa kwa Baraza la Wawakilishi ambapo yeye binafsi aliita ndiyo ngome ya wananchi,” alisema.
Maulid alisema mchango mkubwa wa Jumbe ni kuchangia kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi(CCM) mwaka 1977 baada ya kuvunjwa kwa vyama vya Tanu na ASP na kuzaliwa chama kipya ambacho kimefanikiwa kushika hatamu ya uongozi hadi leo.
Jumbe alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pamoja na Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano kuanzia mwaka 1972 hadi mwaka 1984 wakati alipolazimika kujiuzulu nyadhifa zote kwa sababu za kuchafuka kwa hali ya kisiasa Zanzibar.
Chanzo :swahiba  media
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment