MANARA- SIMBA HATUKUBALI KATU KUONEWA,TUTACHUKUA HATUA STAHILI KWA MARTIN SAANYA ..!!!


UONGOZI wa klabu ya Simba leo unatarajia kuwasilisha rasmi malalamiko yake kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Bodi ya Ligi (TLB) ili imchukulie hatua mwamuzi wa mechi yao dhidi ya Yanga, Martin Saanya. Simba na Yanga zilikutana kwenye Uwanja wa Taifa mwishoni mwa wiki na kutoka sare ya bao 1-1 katika mechi hiyo iliyojaa vurugu.


Vurugu hizo zilitokana na bao la kuongoza la Yanga lililofungwa na Amisi Tambwe ambalo lililalamikiwa kwani kabla hajafunga, mchezaji huyo alishika mpira kwa mkono jambo lililozua vurugu kwa mashabiki wa Simba kwani mapema Ibrahim Ajibu aliifungia Simba bao lililokataliwa na mwamuzi kwa madai alikuwa ameotea.

Mashabiki hao walikwenda mbali kwa kung’oa viti vya uwanja huo na kuvirusha uwanjani.

“Kwa masikitiko makubwa klabu ya Simba imesikitishwa sana na vitendo vilivyofanywa na baadhi ya mashabiki wetu vya kuvunja sehemu ya viti vya Uwanja wa Taifa, kitendo kilichotokea jana (juzi) kwenye mchezo wetu wa Ligi Kuu dhidi ya Timu ya Yanga…

“Sisi tunaamini vitendo viovu vilivyofanywa na mashabiki wetu vilisababishwa na uamuzi wa hovyo kupita kiasi uliosababishwa na waamuzi hao hasa Martin Saanya,” alisema Manara.

“Haieleweki ni kigezo gani mwamuzi huyo alitumia kulikubali goli la 'mpira wa pete'la mshambuliaji wa Yanga, Amisi Tambwe na kulikataa goli halali la mshambuliaji wetu Ibrahim Ajibu.

 Katika mchezo huo vurugu kubwa zilizozuka na kusababisha askari kutumia nguvu ya ziada kwa kutumia mabomu kutuliza vurugu hizo ambazo baadhi ya watu waliumia vibaya. 

Aidha Manara aliomba radhi kwa kitendo cha mashabiki wao kung’oa viti na kusema watawasiliana na mamlaka husika ili walipe
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment