MBWANA SAMATTA AMUULIZIA FARID MUSSA HISPANIA,ASHANGAZWA NA UKIMYA WA AZAM FC..!!!



MSHAMBULIAJI wa Kimataifa wa Tanzania anayechezea klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji, Mbwana Samatta ameonesha kusikitishwa na sintofahamu inayoendelea kuhusu uhamisho wa kiungo mshambuliaji wa Azam FC, Farid Mussa kwenda Hispania kucheza soka ya kulipwa katika klabu ya Teneriffe.

Samatta ambaye pia ni nahodha wa Taifa Stars, ameandika kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram na kusema aliposikia Farid anaenda Hispania kwa majaribio alipata furaha kwa kuamini kwa kipaji chake asingeshindwa kufuzu na furaha yake iliongezeka baada ya kusikia amefuzu.

Pia Samatta aliendela kuandika kuwa alikuwa na furaha kwa sababu aliamini maendeleo ya timu ya taifa yatapiga hatua haraka ikiwa na wachezaji wengi wanaocheza soka la kulipwa nje ya Tanzania.

“Kadri siku zinavyokwenda nimekuwa simsikii Farid kwenye klabu yake ya Teneriffe na habari zilizopo bado yupo Tanzania, Je ni kwa nini bado yupo Tanzania wakati kila kitu kilishakwisha na ni nani mwenye jibu la hili, tahadhari, kuna nini nyuma ya pazia?” Alihoji Samatta.

Farid alikwenda kufanya majaribio katika klabu hiyo inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza nchini humo na kufuzu lakini ameendelea kuwepo nchini huku akiwa hajasajili timu yoyote
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment