Licha
kuisaidia Real Madrid kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA
Champions League) mwaka huu, hilo halijawa sababu kwa staa wa Real
Madrid, Cristiano Ronaldo jina lake kutajwa kuwa tatizo klabuni hapo.
Hilo
limeelezwa na kocha wa zamani wa Real Madrid, Fabio Capello kuwa tangu
kuanza kwa msimu wa 2016/2017, Ronaldo amekuwa katika kiwango kibovu
ambacho kinaweza kuigharimu timu na kufanya vibaya katika michezo yake.
Alisema
yawezekana hali hiyo kwa Ronaldo inajitokeza kutokana na majeruhi
aliyoyapata katika mchezo wa fainali ya Europa wakati Ureno ilipopambana
na Ufaransa, hivyo ni vyema mchezaji huyo akapata muda wa kupumzika ili
kurudi katika ubora wake.
“Tatizo
sasa Real Madrid ni Cristiano Ronaldo,” alisema na kuongeza”Sababu
hayupo katika kiwango kizuri na ndiyo mchezaji wao bora”


0 comments :
Post a Comment