TP Mazembe wamethibitisha Ulimwengu kumaliza mkataba na msimamo wake


Klabu ya TP Mazembe ya Jahmhuri ya Kidemokrasia ya Kongo October 23 2016 ilitangaza rasmi kupitia tovuti ya klabu hiyo kuwa mtanzania Thomas Ulimwengu amemaliza mkataba na TP Mazembe, lakini Ulimwengu hajataka kuongeza mkataba mwingine.
TP Mazembe kupitia tovuti yao wameeleza kuwa Ulimwengu amemaliza mkataba wa miaka mitano wa kuitumikia klabu hiyo, lakini wameweka wazi kuwa walimuhitaji lakini Ulimwengu amekataa kufanya mazungumzo ya kuongeza mkataba na anataka kuondoka.
mazembe
Taarifa iliyoandikwa na tovuti rasmi ya klabu hiyo
Mapema mwaka huu Thomas Ulimwengu aliongea na AyoTV kutoka Lubumbashi na kuweka wazi kuwa anamalizana na TP Mazembe mwishoni mwa mwaka huu, hivyo kwa sasa malengo yake ni kufuata nyayo za rafiki yake Mbwana Samatta kwenda kucheza soka Ulaya.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment