Katika mechi Na. 160 ya Ligi Kuu
ya Vodacom uliozikutanisha timu za JKT Ruvu na Stand United iliyochezwa
Januari 30, mwaka huu kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, Morocco
aliondolewa kwenye benchi (Ordered off) kwa kosa la kupiga maamuzi ya
mwamuzi na kutoa lugha chafu.
Kamati hiyo ya Saa 72 imechukua
hatua hiyo kwa mujibu wa Kanuni ya 40 (11) ya Ligi Kuu kuhusu udhibiti
wa Makocha. Morocco hata kama atakuwa amemaliza mechi tatu nje ya
benchi, hataruhusiwa kukaa kwenye benchi hadi awe amelipa faini hiyo.
Adhabu hiyo ya Morocco itaendelea kumhusu hata kama utakuwa umehamia kwenye timu nyingine na katika msimu mwingine wowote.
..………………………………………………………………………………………………
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


0 comments :
Post a Comment